Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Marko 11:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Yesu na wanafunzi wake wakakaribia kufika Yerusalema, upande wa kijiji cha Betefage na cha Betania, karibu na mulima wa Mizeituni. Yesu akawatuma wawili katika wanafunzi wake,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Marko 11:1
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Daudi aliendelea, akapanda kwenye mulima wa Mizeituni akilia, bila viatu na kichwa chake kimefunikwa. Hata watu wote waliokuwa pamoja naye walifunika vichwa vyao, wakapanda mulima wakilia.


Siku hiyo, atasimama kwenye mulima wa Mizeituni unaokuwa upande wa mashariki wa Yerusalema. Mulima ule utagawanywa kwa sehemu mbili na bonde pana litatokea toka upande wa mashariki mpaka wa magaribi. Nusu moja itaelekea upande wa kaskazini na nusu ingine kusini.


Kisha akawaacha, akatoka inje ya muji wa Yerusalema, naye akaenda Betania na kulala kule.


Basi Yesu alipokuwa akiikaa kwa mulima wa Mizeituni, wanafunzi wake wakamwendea peke yao na kumwuliza: “Utuambie, mambo hayo uliyotoka kusema yatakuwa wakati gani? Na kitambulisho cha kurudi kwako nao wakati wa mwisho wa dunia ni nini?”


Nao walipokwisha kuimba, wakaondoka kwenda kwa mulima wa Mizeituni.


akiwaambia: “Mwende katika kijiji kinachokuwa mbele yenu. Wakati mutakapofika kule, mutaona mwana-punda amefungwa, na hakuna mutu aliyekwisha kupanda juu yake. Mumufungue na kumuleta hapa.


Yesu alipokuwa akiikaa kwa mulima wa Mizeituni kuelekea upande wa hekalu, Petro, Yakobo, Yoane na Andrea walipokuwa peke yao pamoja naye, wakamwuliza:


Basi Yesu akawatuma wawili kati ya wanafunzi wake akiwaambia: “Mwende katika muji, na kule mutakutana mutu mumoja anayebeba mutungi wenye maji. Mumufuate mutu yule,


Aliwaita wanafunzi wake kumi na wawili, akaanza kuwatuma wawili wawili na kuwapatia uwezo wa kufukuza pepo.


Yesu vilevile akajiendea kwa mulima wa Mizeituni.


Kisha mitume wakarudi Yerusalema tokea kwenye mulima wa Mizeituni unaokuwa karibu na muji huo kwenye umbali wa yapata kilometre moja.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ