Marko 10:38 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
38 Lakini Yesu akawaambia: “Hamujui kitu munachoomba. Munaweza kunywa kikombe cha mateso nitakachokunywa? Au munaweza kubatizwa kwa namna ya ubatizo nitakaoupata?”
Mufalme Solomono akamwuliza mama yake: “Kwa nini unataka nimupe Abisagi? Hii ni sawa kabisa na kumutakia ufalme wangu! Kumbuka kwamba yeye ni mukubwa yangu, na si ile tu, kuhani Abiatari na jemadari Yoabu mwana wa Zeruya, wako upande wake!”
Yawe, Mungu wa Israeli, akaniambia hivi: Twaa toka katika mukono wangu kikombe hiki cha divai kinachojaa kasirani yangu uyakunyweshe mataifa yote ninayokutuma kwao.
Wewe unajitakia wewe mwenyewe mambo makubwamakubwa? Usiyatafute! Achana nayo, maana ninaleta maangamizi juu ya wanadamu wote. Pato lako ni hili: nitayaokoa maisha yako kila nafasi utakapokwenda. –Ni ujumbe wa Yawe.
Kisha akajitenga mbali kidogo nao, akainama uso chini. Akaomba akisema: “Ee Baba yangu, kama ikiwezekana, ninakuomba uniondolee mbali kikombe hiki cha mateso. Lakini isikuwe kama vile mimi ninavyotaka, lakini kama vile wewe unavyotaka.”
Akasema: “Ee baba! Yote yanawezekana kwako; ninakuomba uniondolee mbali hiki kikombe cha mateso. Lakini isikuwe kama vile mimi ninavyotaka, lakini kama vile wewe unavyotaka.”
Na ni hivi vilevile Roho wa Mungu anatusaidia katika uzaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba sawa inavyopaswa. Lakini Roho wa Mungu yeye mwenyewe anatuombea kwa Mungu kwa kuugua kusikoweza kuelezwa.