Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Marko 10:32 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

32 Yesu na wanafunzi wake walipokuwa katika njia, wakipanda kwenda Yerusalema, yeye akatangulia mbele yao. Wanafunzi walishikwa na hofu, nao watu waliowafuata waliogopa. Yesu akawatwaa tena wanafunzi wake kumi na wawili, na kuanza kusemezana nao juu ya mambo yatakayomupata.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Marko 10:32
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sasa sikiliza kwa uangalifu, ewe Yoshua, Kuhani Mukubwa; musikilize vilevile enyi makuhani wenzake munaokuwa pamoja naye, ninyi munaokuwa kitambulisho cha wakati muzuri unaokuja: Nitamuleta mutumishi wangu anayeitwa Tawi.


Katika siku zile Yesu akasema: “Ee Baba, Mwenyeji wa mbingu na dunia, ninakushukuru kwa maana mambo uliyoyaficha kwa watu wenye hekima na elimu, umeyafunua kwa wanaokuwa wadogo.


Akawajibu: “Ninyi mumefunuliwa kujua siri ya Ufalme wa mbinguni, lakini kwao si vile.


Watu wote wakashangaa sana na kuulizana: “Hatujaona mambo kama haya! Hakika mafundisho haya ni yenye mamlaka! Mutu huyu anaamuru hata pepo, nao wanamutii!”


Hakusema nao pasipo kutumia mifano lakini alipokuwa pamoja na wanafunzi wake peke yao, aliwafasiria mambo yote.


Kisha Yesu akawageukia wanafunzi wake wakiwa peke yao, akawaambia: “Heri watu wanaoona mambo yale munayoona!


Kisha kusema maneno hayo, Yesu akatembea mbele ya kundi la watu kwenda Yerusalema.


Siku za Yesu za kunyanyuliwa mbinguni zikakaribia. Kwa hiyo akakusudia sana kwenda Yerusalema,


Basi Toma, anayeitwa “Pacha,” akawaambia wanafunzi wenzake: “Nasi tuende vilevile, tukufie pamoja naye.”


Wanafunzi wakamwambia: “Mwalimu, hakujapita siku nyingi tokea pale Wayuda walipotaka kukutupia mawe, na sasa unataka kwenda tena kule!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ