Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Marko 10:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Yesu akamwangalia kwa upendo, akamwambia: “Unakosewa na kitu kimoja tu: kwenda uuzishe vitu vyote unavyokuwa navyo, na uwape wamasikini mali zile, nawe utakuwa na akiba mbinguni. Kisha urudi, unifuate!”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Marko 10:21
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kijana yule hakusita hata kidogo kutimiza sharti hilo, kwa vile alivyomupenda binti ya Yakobo, ingawa ni yeye ndiye aliyeheshimika kuliko wote katika nyumba yao.


Nunua ukweli, wala usiuuzishe; nunua hekima, mafundisho na akili.


Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Kama mutu akitaka kunifuata, ajikane yeye mwenyewe, lakini ajitolee kwa kubeba musalaba wake na kunifuata.


Yesu akamujibu: “Ukitaka kuwa mutimilifu, kwenda uuzishe vitu unavyokuwa navyo, na uwape wamasikini mali zile, nawe utakuwa na akiba mbinguni. Kisha urudi, unifuate.”


Lakini kijana yule aliposikia maneno yale, alikunja uso, na kujiendea katika huzuni, kwa sababu alikuwa tajiri sana.


Kisha Yesu akaita kundi la watu pamoja na wanafunzi wake, na kuwaambia: “Kama mutu akitaka kunifuata, asijishugulikie mwenyewe, lakini ajitolee kwa kubeba musalaba wake na kunifuata.


Kuna kitu kimoja tu cha lazima. Maria amechagua kitu kinachokuwa kizuri zaidi ambacho hakuna mutu atakayekiondoa kwake.”


Muuzishe vitu munavyokuwa navyo, muwasaidie wamasikini. Mujiwekee feza zisizoweza kuwa na upungufu, nayo akiba isiyoweza kumalizika katika mbingu. Kule wizi hawawezi kukaribia wala nondo hawaharibu.


Yesu akaongeza kusema: “Nami ninawaambia: mutumie mali ya dunia hii kwa kuunga urafiki, kusudi wakati mali ile itakapokosekana, mupate kupokelewa kwenye makao ya milele.


Yesu aliposikia maneno haya, akamwambia: “Ungali unakosewa na kitu kimoja tu: uuzishe vitu vyote unavyokuwa navyo, na uwape wamasikini mali zile, nawe utakuwa na akiba mbinguni. Kisha urudie unifuate!”


Yesu alipokaribia muji wa Yerusalema, na alipouona, akaulilia,


Kisha akawaambia wote: “Kama mutu akitaka kunifuata, asijishugulikie mwenyewe, lakini ajitolee kwa kubeba musalaba wake kila siku na kunifuata.


Kama mutu akitaka kunitumikia, anapaswa kunifuata, na hivi mutumishi wangu atakuwa popote nitakapokuwa. Mutu akinitumikia, Baba yangu atamupa heshima.


Nimewaambia maneno haya kusudi mukuwe na amani, mukibaki katika umoja nami. Mutapata mateso katika dunia. Lakini mujipe moyo, kwa kuwa mimi nimepata ushindi juu ya vyote katika dunia.”


Waliuzisha mali zao na vyote walivyokuwa navyo na kugawanya kati yao kufuatana na mahitaji ya kila mutu.


Kwa ngambo yangu, nitafurahi kutumia vyote ninavyokuwa navyo na kujitoa mimi mwenyewe, kwa ajili yenu. Ikiwa ninawapenda zaidi namna hii, hamupaswi kupungukiwa na upendo kwangu.


Nao wote wanaotaka kuishi maisha ya kumwabudu Mungu katika kuungana na Kristo Yesu, watateswa.


Muliwahurumia wale waliokuwa katika kifungo, nanyi mulikubali kwa furaha kunyanganywa mali zenu, kwa sababu mulijua kwamba muko na mali inayokuwa bora zaidi na yenye kudumu.


Kwa maana mutu akivunja agizo moja tu la Sheria, yeye anavunja Sheria yote.


Lakini niko na neno hili juu yako: kati yako kuna watu wamoja wanaoshika mafundisho ya Balama. Huyu ndiye aliyemufundisha Balaka kwamba awapime Waisraeli, kusudi wakule vyakula vya kutambikia sanamu za miungu na kufanya uasherati.


Lakini niko na neno hili juu yako: unamuvumilia yule mwanamuke Yezebeli, anayejiita kuwa nabii wa Mungu. Yeye anawapotosha watumishi wangu akiwafundisha kufanya uasherati na kula nyama za kutambikia sanamu za miungu.


Lakini niko na neno moja juu yako: wewe hauna tena upendo kwangu kama vile mbele.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ