Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Ninachukia kuachana. Ninachukia wakati mumoja wenu anapomutendea muke wake ubaya ule. Muhakikishe kwamba hakuna hata mumoja wenu anayekosa uaminifu kwa muke wake.
“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munawafungia watu wengine njia ya kuingia katika Ufalme wa mbinguni. Ninyi wenyewe hamwingii mule na zaidi ya hii munawazuiza wale wanaotaka kuingia. [
Yesu akaondoka kule, akaenda katika jimbo la Yudea na kuvuka ngambo ingine ya Yordani. Na makundi mengi ya watu wakakusanyika tena mbele yake, naye akaanza kuwafundisha, kama vile alivyozoea kufanya.
Wafarisayo wakamufikia Yesu na kuanza kubishana naye. Wakamupima wakimwomba awaonyeshe kitambulisho kinachohakikisha kwamba uwezo wake umetoka kwa Mungu.
Wafarisayo na walimu wa Sheria wa kikundi chao wakawanungunikia wanafunzi wake, wakisema: “Kwa sababu gani munakula na kunywa pamoja na walipishaji wa kodi na watenda mabaya?”
Walimu wa Sheria na Wafarisayo wakamuchunguza Yesu kusudi waone kama ataponyesha mutu kwa siku ya Sabato. Walifanya vile kusudi wapate sababu ya kumushitaki.