Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Marko 10:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Yesu akaondoka kule, akaenda katika jimbo la Yudea na kuvuka ngambo ingine ya Yordani. Na makundi mengi ya watu wakakusanyika tena mbele yake, naye akaanza kuwafundisha, kama vile alivyozoea kufanya.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Marko 10:1
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, zaidi ya kuwa na hekima yake, Muhubiri aliendelea kuwafundisha watu ujuzi. Alipima, akachunguza na kutia kwa usawa mezali kwa ufundi mwingi.


Wao walinigeuzia mugongo pahali pa kunigeuzia nyuso zao; ingawa nimewafundisha tena na tena, wao hawakusikiliza na kuyapokea mafundisho yangu.


Kisha Yesu akawaambia watu wale: “Mumekuja na panga na magongo kwa kunikamata kama watu wanavyokwenda kumukamata munyanganyi? Siku zote niliikaa ndani ya hekalu, nikifundisha, nanyi hamukunikamata.


Yesu alizunguka katika Galilaya yote akifundisha katika nyumba zao za kuabudia, akihubiri Habari Njema ya Ufalme. Aliponyesha watu waliokuwa na magonjwa yote na uzaifu wa kila namna.


Yesu na wanafunzi wake walienda Kapernaumu. Siku ya Sabato ilipotimia, Yesu akaingia katika nyumba ya kuabudia na kufundisha watu.


Wafarisayo wamoja wakamufikia kwa kumupima, wakamwuliza: “Sheria yetu inamuruhusu mutu kufukuza muke wake?”


Yesu alipokuwa akifundisha katika hekalu akauliza: “Namna gani walimu wa Sheria wanaweza kusema kwamba Kristo ni Mwana wa Daudi?


Siku zote nilikuwa pamoja nanyi, nami nilifundisha ndani ya hekalu, nanyi hamukunikamata. Lakini mambo haya yamefanyika kusudi Maandiko Matakatifu yatimizwe.”


Yesu akaenda tena pembeni ya ziwa la Galilaya. Kundi kubwa la watu wakamufikia, naye akawafundisha.


Yesu akawafundisha mambo mengi akitumia mifano. Yeye akawaambia hivi katika mafundisho yake:


Siku ya Sabato ilipotimia, akaanza kufundisha katika nyumba ya kuabudia. Watu wengi waliomusikiliza, wakashangaa sana na kuulizana: “Huyu amepata maneno haya yote kutoka wapi? Ni hekima ya namna gani aliyopata? Ni kwa uwezo wa namna gani anafanya miujiza kama hii?


Wakati Yesu alipotoka ndani ya chombo, akaona kundi kubwa la watu, akawasikilia huruma, kwa sababu walikuwa kama kondoo wasiokuwa na muchungaji. Basi akaanza kuwafundisha maneno mengi.


Naye alishangaa sana kwa sababu ya kutokuamini kwa watu wale. Kisha Yesu akazunguka katika vijiji vya kandokando akiwafundisha watu.


Halafu Yesu akaenda tena ngambo ingine ya Yordani, pahali Yoane alipobatiza watu zamani, na kubaki kule.


Kisha akawaambia wanafunzi wake: “Turudi Yudea.”


Yesu akamujibu: “Nilisema na watu wote waziwazi, nilifundisha siku zote katika nyumba za kuabudia na katika hekalu, pahali Wayuda wote wanapokutana. Sikusema kitu kwa uficho.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ