Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Marko 1:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Mimi nimewabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mutakatifu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Marko 1:8
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Musikilize maonyo yangu; nitawamiminia mawazo yangu, nitawajulisha maneno yangu.


Hali itaendelea kuwa hivyo mpaka tujazwe Roho wa Mungu kutoka juu. Hapo jangwa litakuwa shamba lenye udongo muzuri tena, na mashamba yenye udongo muzuri yatakuwa pori.


Nitaimwangilia maji inchi yenye kiu, na kutiririsha muto katika inchi iliyokauka. Nitajaza roho wangu juu ya wazao wako, nitawamwangia watoto wako baraka yangu.


Mimi ninawabatiza kwa maji kwa kuonyesha kwamba mumegeuka toka zambi zenu. Lakini yule atakayekuja nyuma yangu atawabatiza kwa Roho Mutakatifu na kwa moto. Yeye ni mwenye uwezo kunipita, nami sistahili hata kumuvua viatu.


Yeye alihubiri hivi kwa watu: “Yule anayekuja nyuma yangu ni mwenye uwezo kunipita; nami sistahili hata kuinama na kufungua kamba ya viatu vyake.


Katika siku zile, Yesu akatoka Nazareti, katika Galilaya, akabatizwa na Yoane katika Yordani.


Basi Yoane akawaambia wote: “Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yule atakayekuja nyuma yangu ni mwenye uwezo kunipita; nami sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mutakatifu na kwa moto.


Yoane akawajibu: “Mimi ninabatiza kwa maji, lakini kati yenu kuna mutu ninyi musiyemujua,


Mimi sikumujua ni nani, lakini yule aliyenituma kubatiza kwa maji aliniambia: ‘Yule utakayemwona Roho akishuka juu yake na kukaa juu yake, mutu yule ndiye anayebatiza kwa Roho Mutakatifu.’


Kwa maana Yoane alibatiza kwa maji, lakini kisha siku chache, ninyi mutabatizwa kwa Roho Mutakatifu.”


Na wale wanafunzi Wayuda waliofika pamoja na Petro wakashangaa sana kwa kuona kwamba Mungu ametoa zawadi ya Roho wake Mutakatifu kwa watu wa mataifa mengine vilevile.


‘Mungu anasema: Katika siku za mwisho, nitashusha Roho wangu juu ya watu wote; wana wenu na wabinti zenu watatabiri, vijana wenu wataona maono nao wazee wenu wataota ndoto.


Wote wakapewa Roho Mutakatifu na kuanza kusema kwa luga mbalimbali kwa kadiri Roho alivyowawezesha kusema.


Vilevile sisi wote, Wayuda na watu wa mataifa mengine, watumwa na watu wanaokuwa huru, tumebatizwa kwa Roho mumoja kusudi tukuwe mwili mumoja na sisi wote tumekunyweshwa Roho mumoja.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ