Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Marko 1:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Watu wengi walitoka katika Yerusalema na katika jimbo lote la Yudea kwa kumwendea Yoane. Walikubali zambi zao, naye akawabatiza katika muto Yordani.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Marko 1:5
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha niliitikia makosa yangu mbele yako, wala sikuficha uovu wangu. Nilisema kwamba nitaungama makosa yangu mbele ya Yawe. Nawe ukanisamehe zambi yangu.


Anayeficha makosa yake hatafanikiwa, lakini anayeungama na kuyaacha atahurumiwa.


Makundi mengi ya watu yakamufuata kutoka Galilaya, inchi ya Miji Kumi, Yerusalema, Yudea, na toka ngambo ya mashariki ya muto Yordani.


Hivi Yoane alitokea katika jangwa, akibatiza watu, akiwahubiri kwamba wageuke toka zambi zao, wabatizwe, na Mungu atawasamehe.


Yoane alikuwa akivaa nguo iliyotengenezwa na manyoya ya ngamia na mukaba wa ngozi katika kiuno. Naye alikuwa akikula nzige na asali ya pori.


Mambo hayo yalifanyika Betania, ngambo ya muto Yordani, pahali Yoane alipokuwa akibatiza.


Yoane vilevile alikuwa akibatiza kule Ainoni, karibu na Salimu, kwa sababu kule kulikuwa maji mengi. Watu walimwendea, naye akawabatiza.


Yoane alikuwa kama taa inayowaka na kuangaza, na ninyi mulipendezwa kufurahishwa na mwangaza wake kwa muda.


Wengi kati ya wale walioamini walikuja kuungama na kutangaza waziwazi mambo waliyofanya.


Petro akawajibu: “Mugeuke toka katika zambi zenu, na kila mumoja wenu abatizwe kwa jina la Yesu Kristo, na Mungu atawasamehe zambi zenu. Hivi mutapokea zawadi ya Roho Mutakatifu.


Basi muitikiane zambi ninyi kwa ninyi na kuombeana kusudi mupate kuponyeshwa. Maombi ya bidii ya mwenye haki ni yenye faida kubwa.


Yoshua akamwambia Akana: “Mwana wangu, umutukuze Yawe, Mungu wa Israeli, umusifu na kisha uniambie yale uliyotenda, wala usinifiche.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ