43 Pale pale Yesu akamwagiza kwa nguvu aende na kusema:
Nayo macho yao yakapona. Na Yesu akawaagiza kwa nguvu, akisema: “Angalisho, musimujulishe hata mutu mumoja jambo hili.”
Na mara moja mutu yule akapona ukoma na kutakaswa.
“Angalisho, usimwambie mutu hata neno moja juu ya hii. Lakini kwenda kwa kuhani na kumwonyesha jinsi unavyokuwa sasa. Kisha utoe sadaka kama Musa alivyoamuru, kuwa ushuhuda kwa wote kwamba umetakaswa.”
Lakini Yesu aliwakaripia kwa nguvu wasimutambulishe yeye ni nani.
Lakini Yesu aliwaagiza sana wasimwambie mutu yeyote jambo lililofanyika. Kisha akawaambia wamupe mutoto yule chakula.
Yesu akawaagiza wasimwambie mutu habari ya tendo hili. Lakini kwa kadiri alivyowakataza, wao walizidi kutangaza habari.
Wazazi wake wakashangaa sana na Yesu akawaagiza wasimwambie mutu yeyote yale yaliyotokea.