Marko 1:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
34 Yesu akawaponyesha watu wengi wenye magonjwa mbalimbali. Vilevile alifukuza pepo wengi, wala hakuwaachilia pepo kusema neno, kwa sababu walimujua yeye ni nani.
Yesu alizunguka katika Galilaya yote akifundisha katika nyumba zao za kuabudia, akihubiri Habari Njema ya Ufalme. Aliponyesha watu waliokuwa na magonjwa yote na uzaifu wa kila namna.
Habari zake zikavuma katika inchi yote ya Suria. Wakamuletea watu wote walioteswa na magonjwa mbalimbali na wenye maumivu ya kila namna, wenye pepo, wenye kifafa na wenye kupooza, naye Yesu akawaponyesha.
Pepo wakatoka ndani ya watu wengi, wakilalamika, wakisema: “Wewe ni Mwana wa Mungu!” Lakini Yesu akawakaripia, na hakuwaachilia waseme neno, kwa sababu walijua kwamba yeye ndiye Kristo.