31 Basi Yesu akajongea karibu naye, akamushika mukono na kumusimamisha. Naye akapona homa na kuanza kuwashugulikia.
Nitamurudishia Yawe nini, kwa vyote alivyonitendea?
Pale kulikuwa vilevile wanawake wengi walioangalia kwa mbali; ndio wale waliomufuata Yesu tokea Galilaya, wakimushugulikia.
Mama mukwe wa Simoni alikuwa katika kitanda, kwa sababu alikuwa na homa. Wakati Yesu alipofika pale, mara moja wakamupasha habari ya ugonjwa wake.
Ilipokuwa magaribi, jua lilipokuwa limekwisha kutua, wakamuletea Yesu watu wote waliokuwa wagonjwa na waliokuwa na pepo.
Wanawake hawa ni wale waliomufuata Yesu na kumushugulikia wakati alipokuwa Galilaya. Wanawake wengine wengi waliomufuata mpaka Yerusalema walikuwa pale vilevile.
Akashika mukono wa mutoto, akamwambia: “Talita kumu,” maana yake: “Kijana binti, ninakuambia, amuka!”
Petro akamushika mukono na kumusimamisha wima. Kisha akawaita wanafunzi na wajane, akamupeleka mbele yao akiwa muzima.