Yesu alizunguka katika Galilaya yote akifundisha katika nyumba zao za kuabudia, akihubiri Habari Njema ya Ufalme. Aliponyesha watu waliokuwa na magonjwa yote na uzaifu wa kila namna.
Yesu na wanafunzi wake walipotoka ndani ya ile nyumba ya kuabudia, mara moja wakaenda kwa nyumba ya Simoni na Andrea, wakiwa pamoja na Yakobo na Yoane.
Yesu akaondoka kule, akaenda katika jimbo la Yudea na kuvuka ngambo ingine ya Yordani. Na makundi mengi ya watu wakakusanyika tena mbele yake, naye akaanza kuwafundisha, kama vile alivyozoea kufanya.
Siku ya Sabato ilipotimia, akaanza kufundisha katika nyumba ya kuabudia. Watu wengi waliomusikiliza, wakashangaa sana na kuulizana: “Huyu amepata maneno haya yote kutoka wapi? Ni hekima ya namna gani aliyopata? Ni kwa uwezo wa namna gani anafanya miujiza kama hii?
Yesu akafika Nazareti, nafasi alipokomalia. Siku ya Sabato ilipotimia akaingia katika nyumba ya kuabudia kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama kwa kusoma Maandiko Matakatifu;
Yesu akawaambia: “Hakika mutaniambia fumbo hili: ‘Muganga, ujiponyeshe wewe mwenyewe!’ Na vilevile mutaniambia hivi: ‘Tumesikia mambo yote uliyotenda katika muji Kapernaumu, basi uyafanye hapa vilevile katika muji wako.’ ”
Na sawa ilivyokuwa desturi, Paulo akaingia katika nyumba ile. Kwa muda wa siku tatu za Sabato zilizofuatana juma kwa juma, akabishana na watu waliokuwa mule, akitumia Maandiko Matakatifu.