Halafu, Elisha akawaacha ngombe wake, akamufuata Elia mbio na kumwambia: “Uniruhusu kwanza niende kumupa baba yangu na mama yangu busu la kwa heri, kisha nikufuate.” Elia akamujibu: “Kwenda! Ni nini niliyokutendea?”
“Yeye anayemupenda baba yake au mama yake kuliko mimi, hastahili kuwa wangu, na yeyote anayemupenda mwana wake au binti yake kuliko mimi hastahili kuwa wangu vilevile.
Yesu alipoendelea mbele kidogo, akawaona wandugu wengine wawili: Yakobo na Yoane waliokuwa wana wa Zebedayo. Walikuwa ndani ya chombo wakitengeneza nyavu zao.
Yesu akajibu: “Kweli ninawaambia: kama mutu akiacha nyumba yake, ndugu, dada, mama, baba, watoto wake au mashamba yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Habari Njema,
“Mutu anayenifuata, atakuwa kweli mwanafunzi wangu kama akinipendelea mimi kuliko baba na mama yake, muke na watoto wake, wakaka na wadada zake. Na zaidi ya hii hapaswi kujipendelea yeye mwenyewe vilevile.
Kwa hiyo basi, tangu sasa hatumuhesabu tena mutu yeyote kufuatana na hali ya kimutu. Hata ikiwa tulimuhesabu Kristo kufuatana na hali ya kimutu, kwa sasa hatumuhesabu tena kufuatana na hali ile.