Ee Yawe, umekataa Yuda kabisa? Moyo wako umechukizwa na Sayuni? Kwa nini umetupiga vibaya kama hivi, hata hatuwezi kupona tena? Tulitazamia kupata amani, lakini hakuna kitu kizuri. Tulitazamia kupona, lakini tumepatwa na vitisho.
Kwa hiyo Yawe akaniambia: Wewe mwanadamu! Mifupa hiyo ni mufano wa watu wote wa inchi ya Israeli. Wao, wanasema: Mifupa yetu imekauka, matumaini yetu yamepotea nasi tumekwisha kabisa.