Uovu wako utakuazibu; na uasi wako utakuhukumu. Ujue na kutambua kwamba ni vibaya sana kuacha Bwana wako Yawe, Mungu wako, na kutokuwa na woga wangu ndani yako. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi.–
Nao walifika, wakaitwaa na kuirizi. Lakini wao hawakukusikiliza, wala hawakufuata sheria zako. Hawakutenda mambo uliyoamuru. Ndiyo maana utawafanya wapatwe na hasara hii.
Wewe Yuda, hayo yote yamekupata kwa ajili ya mwenendo na matendo yako. Hiyo ndiyo hasara inayokufikia, tena ni yenye uchungu; yamepenya mpaka ndani ya moyo wako.
Namna gani muji uliokuwa umejaa watu, sasa unakaa peke yake! Ulikuwa na utukufu kati ya mataifa, sasa umekuwa kama mama mujane. Ulikuwa kama binti wa mufalme kati ya miji, sasa umekuwa mutumwa.
Lakini Yawe amefanya sawa kwa maana nimeliasi neno lake. Munisikilize enyi watu wote, muyaangalie mateso yangu. Wabinti zangu na vijana wangu wanaume wamepelekwa katika utumwa.
Ona, ee Yawe, ninavyokuwa tabani. Roho yangu imechafuka, moyo wangu unaugua maana nimekuasi vibaya. Kule inje kumejaa mauaji, ndani nako ni kama kifo tu.
Muji Yerusalema ulitenda zambi kubwa, ukakuwa muchafu kwa ajili ya zambi zake. Wote waliousifia wanauzarau, maana wameuona uchi wake. Muji wenyewe unaugua na kujificha kwa ajili ya haya.
Kwa hasira yake, Yawe amewaweka watu wa Sayuni katika giza. Ametupa toka mbinguni mpaka katika dunia utukufu wa Israeli. Kwa siku ya hasira yake, alilitupilia mbali hata hekalu lake.
Mufalme wa Babeli anasimama kwa mwanzo wa hizo njia mbili, kwenye masanganjia, apate kuaguza. Anatikisa mishale, anauliza shauri la sanamu ya miungu yake na kuchunguza maini ya nyama.
Usiogope mateso utakayopata. Sikiliza, Shetani atawajaribu kwa njia ya kuwatia wamoja wenu katika kifungo, nanyi mutateseka kwa muda wa siku kumi. Lakini ukuwe mwaminifu mpaka kufa, nami nitakupatia taji ya uzima.
Hivyo, Waisraeli wote wakakusanyika kule Misipa. Walichota maji na kuyamimina mbele ya Yawe, wakafunga kula chakula siku ile yote na kusema: “Tumetenda zambi mbele ya Yawe.” Samweli akakuwa mwamuzi wa Waisraeli kule Misipa.