Lakini sasa watu wananichekelea, tena watu wanaokuwa wadogo kuliko mimi; watu ambao niliwaona baba zao hawafai hata kuwahesabu kama imbwa wangu wakilinda kondoo.
Maana Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nitazikomesha kabisa kutoka pahali hapa sauti za furaha na shangwe, nazo nyimbo za wenye kufanya ndoa. Nitayafanya hayo yote katika nyakati zenu, na mutayaona waziwazi.
Inchi itakuwa jangwa na katika miji ya Yuda na barabara za Yerusalema nitakomesha sauti zote za furaha na shangwe, nazo nyimbo za wenye kufanya ndoa, kwa sababu inchi itakuwa ukiwa.
Niliwaita wapenzi wangu, lakini wao wakanidanganya. Makuhani na wazee wangu wamekufia katika muji, wakijitafutia chakula kusudi wajirudishie nguvu zao.
Barabara za Sayuni zinaomboleza, maana hakuna anayepita kwa sikukuu. Milango yake yote ni tupu, makuhani wake wanaugua, wabinti zake wana huzuni, na muji wenyewe uko katika uchungu.
Sauti ya wapiga vinubi na ya wapiga vinanda, ya wapiga filimbi na ya baragumu, haitasikilika ndani yako tena. Fundi wa kazi yoyote hataonekana ndani yako tena hata kidogo wala kelele la jiwe la kusagia halitasikilika.