Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Maombolezo 5:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Ukumbuke, ee Yawe, mambo yaliyotupata! Utuangalie, uone haya yetu!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Maombolezo 5:1
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wao wakaniambia: “Wayuda walioponyoka na kubaki katika jimbo lile, wako katika taabu nao wanazarauliwa. Ukuta wa Yerusalema umebomolewa na milango yake imeteketezwa.”


Kumbuka sasa lile ulilomwambia mutumishi wako Musa, uliposema: ‘Kama hamutakuwa waaminifu, nitawatawanya kati ya mataifa.


Watu wa Yuda wakakuwa wanalalamika wakisema: “Tunachoka na kubeba mizigo na bado kuna takataka nyingi za kubeba. Hatuwezi kuendelea kujenga ukuta.”


Kumbuka kwamba uliniumba kwa udongo. Utanirudisha tena katika mavumbi?


Kumbuka, maisha yangu ni pumzi tu; jicho langu halitaona jambo zuri lolote tena.


Uangalie mateso yangu, uniokoe, kwa maana sikusahau sheria yako.


Kumbuka, ee Yawe, mazarau ya waadui zako; taifa pumbafu linatukana jina lako.


Ee Bwana, uwalipize mataifa jirani mara saba kwa ajili ya matusi waliyokutukana.


Tunazarauliwa na mataifa jirani, jirani zetu wanatuchekelea na kutusimanga.


Juu ya kuta zako, ee Yerusalema, nimeweka walinzi, usiku na muchana hawatakaa kimya hata kidogo. Enyi munaomukumbusha Yawe ahadi yake, musikae kimya;


Nami nikasema: Lakini wewe Yawe unanielewa vizuri; unikumbuke na kuja kunisaidia. Unilipizie watesaji wangu kisasi. Wewe ni muvumilivu, usiniache niangamie; kumbuka kwamba ninatukaniwa kwa ajili yako.


Ninyi munasema: Tumepatishwa haya na kutukaniwa; haya imefunika nyuso zetu, kwa sababu wageni wameingia katika sehemu takatifu za nyumba ya Yawe.


Watu wa Yerusalema wote wanaugua, wakitafuta chakula; wanatoa vitu vyao vya bei kali kwa kupata chakula, kusudi wajirudishie nguvu zao. Nao muji unalia, Ee Yawe, uniangalie, ona jinsi nilivyogeuka kuwa zaifu.


Ona, ee Yawe, ninavyokuwa tabani. Roho yangu imechafuka, moyo wangu unaugua maana nimekuasi vibaya. Kule inje kumejaa mauaji, ndani nako ni kama kifo tu.


Uchafu wake ulionekana waziwazi, lakini muji wenyewe haukujali mwisho wake. Anguko lake lilikuwa kubwa sana; hakuna anayeweza kuufariji. Unasema: Angalia, ee Yawe, mateso yangu, maana adui yangu ameshinda.


Wapita njia wote wanakuchekelea; wanakupigia muunzi, ee Yerusalema, wakitikisa vichwa vyao kwa mazarau na kusema: Huu ndio ule muji uliofikia ukamilifu wa uzuri, muji uliokuwa furaha ya dunia nzima?


Angalia, ee Yawe, uone! Kuna yeyote uliyemutendea kama ulivyotutendea sisi, hata wamama wawakule watoto wao nao makuhani wauawe ndani ya hekalu lako?


Kukumbuka taabu na kutangatanga kwangu kunanipa uchungu na sumu.


mpaka Yawe kutoka kule mbinguni aangalie chini na kuona.


Umesikia matukano yao, ee Yawe, na mipango yao yote juu yangu.


Ee Yawe, nimesikia juu ya utukufu wako, juu ya matendo yako, nami ninaogopa. Uyafanye tena mambo yale wakati wetu; uyafanye yajulikane wakati huu wetu. Unapokasirika tafazali ukumbuke huruma yako!


Na akaongeza kusema: “Ee Yesu, usinisahau wakati utakapokuja katika ufalme wako!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ