Maombolezo 4:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
21 Wakaaji wa Edomu, ile inchi ya Uzi, mushangilie na kufurahi kwa sasa. Lakini kikombe hiki cha azabu kitawafikia vilevile. Mutakikunywa na kulewa, hata mutavaa uchi!
Ee Yawe, usisahau mambo Waedomu waliyotenda, siku ile Yerusalema iliponyanganywa; kumbuka maneno haya waliyosema: “Mubomoe Yerusalema! Muongoe hata na misingi yake!”
Ewe kijana, furahia ujana wako, moyo wako ukuwe na raha wakati ungali kijana. Fuata mapenzi ya moyo wako na tamaa ya macho yako. Lakini kumbuka kwamba Mungu atakuhukumu kadiri ya hayo yote.
Yawe anasema hivi: Ikiwa wale ambao hawakustahili kunywa kikombe cha azabu ni lazima wakikunywe, basi, wewe utaachwa bila kuazibiwa? Hapana! Hautakosa kuazibiwa; ni lazima ukunywe hicho kikombe!
Wewe mwanadamu! Watu wa muji wa Tiro wameuchekelea Yerusalema na kusema: Aha! Yerusalema muji ambao watu wote walipitia, umeangamizwa! Sasa umetuachia nafasi; utajiri wake umeharibika!
Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Edomu, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamewawinda wandugu zao Waisraeli kwa mapanga, wakaitupilia mbali huruma yao yote ya kindugu. Hasira yao haikuwa na mwisho, waliiacha iwake siku zote.
Haya ni maono ya Obadia. Bwana wetu Yawe anasema hivi juu ya taifa la Edomu. Tumepata habari kutoka kwa Yawe; mujumbe ametumwa kati ya mataifa: Musimame! Tuende tupigane na taifa la Edomu!
Enyi wakaaji wa Safiri, muende mukiwa uchi na wenye haya. Wakaaji wa Zanana musitoke inje ya muji wenu. Watu wa Beti-Ezeli wanalia; musaada wao kwenu umeondolewa.
“Sikiliza, ninakuja kwa saa isiyozaniwa kama vile mwizi. Heri yule anayekesha na kutunza nguo zake vizuri kusudi asitembee uchi na kujifezehesha mbele ya watu.”