Nitaita wavuvi wengi kuja kuwanasa watu hawa. Kisha, nitaita wawindaji wengi kuja kuwawinda juu ya kila mulima, kila kilima na katika mapango ya chini ya mawe.
Alipokuwa katika mulango wa Benjamina, mulinzi mumoja anayeitwa Iria mwana wa Selemia, mujukuu wa Hanania, alimukamata Yeremia na kumwambia: Wewe unatoroka kusudi uende kujiunga na Wakaldea!
manabii wanatabiri mambo ya uongo, nao makuhani wanatafuta faida yao wenyewe; nao watu wangu wanaona jambo hilo kuwa sawa. Lakini mwisho wake utakapofika mutafanya nini?
Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Babeli ni kama uwanja wa kupepetea ngano wakati unapotayarishwa. Lakini bado kidogo tu, wakati wa mavuno utaufikia.
Naye Yawe akaniuliza: Amosi, unaona nini? Nami nikamujibu: Ninaona kikapu cha matunda yenye kuivya. Kisha Yawe akaniambia: Mwisho umewafikia watu wangu wa Israeli. Sitavumilia tena maovu yao.