Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Maombolezo 4:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Yawe mwenyewe aliwatawanya, wala hatawajali tena. Makuhani hawaheshimiwi tena, wazee hawapendelewi tena.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Maombolezo 4:16
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ninalaani hasira yao kali sana na kasirani yao isiyokuwa na huruma. Nitawatawanya katika inchi ya Yakobo, nitawasambaza katika inchi ya Israeli.


Kwa hiyo, Yawe alimuleta mufalme wa Wakaldea ambaye aliwaangamiza vijana wao kwa upanga hata ndani ya Pahali Patakatifu; wala hakumuhurumia mutu yeyote akuwe kijana au binti, muzee au muzaifu. Wote Yawe aliwatia katika mikono yake.


atawatawanya wazao wao kati ya watu, na kuwasambaza katika dunia yote.


Hata hivyo Mungu aliona taabu yao, wakati aliposikia kilio chao;


Kila mutu atapatwa na mambo yaleyale: mutu wa kawaida na kuhani; mutumwa na bwana wake; mujakazi na bibi wake; mwenye kununua na mwenye kuuzisha; mukopeshaji na mukopaji; mwenye kudai na mwenye kudaiwa.


Niliwakasirikia watu wangu, Israeli, nikawafanya watu wangu kuwa wanaharamu. Niliwatia katika mikono yako, nawe haukuwaonea huruma; na wazee uliwabebesha nira nzito sana.


Nitawafanya kuwa kitu cha kutisha kwa falme zote za dunia, kwa sababu ya mambo ambayo Manase mwana wa Hezekia, aliyofanya kule Yerusalema, alipokuwa mufalme wa Yuda. –Ni ujumbe wa Yawe.


Nitawafanya kuwa kitu cha kuchukiza mbele ya falme zote za dunia. Watakuwa kitu cha zihaka, kitu cha kuzomewa, kuchekelewa na kulaaniwa kila fasi nitakapowasambaza.


Kisha Nebuzaradani mukubwa wa waaskari walinzi wa mufalme, alimukamata Seraya Kuhani Mukubwa, na Zefania kuhani wa pili, pamoja na walinda mulango watatu;


Angalia, ee Yawe, uone! Kuna yeyote uliyemutendea kama ulivyotutendea sisi, hata wamama wawakule watoto wao nao makuhani wauawe ndani ya hekalu lako?


Amelibomoa hekalu lake kama kibanda katika bustani, ameharibu pahali pake pa kusanyiko. Amefanya sikukuu na siku ya Sabato visahauliwe kule Sayuni, kwa hasira yake kubwa amewakataa mufalme na makuhani.


Wakubwa wetu wametundikwa kwa mikono yao; wazee wetu hawapewi heshima yoyote.


Hukohuko katika muji wazazi watawakula watoto wao wenyewe na watoto watawakula wazazi wao. Nitatimiza hukumu zangu juu yenu na watakaobaki wazima nitawasambaza pande zote.


“Yawe atawafanya mushindwe na waadui zenu. Ninyi mutakwenda kuwashambulia kwa njia moja, lakini mutawakimbia kwa njia saba. Nanyi mutakuwa kinyaa kwa watu wote katika dunia.


Ningaliwaangamiza kabisa na kuwafanya wasikumbukwe tena na mutu yeyote,


Agano lile halitakuwa sawa na lile nililofanya na babu zao siku nilipowakamatia kwenye mukono na kuwaondoa toka inchi ya Misri. Kwa sababu hawakushika lile agano, kwa hiyo vilevile sikuwashugulikia. Ni Bwana wetu Mungu anayesema hivyo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ