Kwa nini munapiga kelele za shangwe, na muji wote umechangamuka na kujaa vigelegele? Watu wenu waliokufa hawakuuawa katika vita, wala hawakuuawa katika mapigano.
Lakini Yawe anasema: Munafikiri kwamba mama anaweza kumusahau mutoto anayemunyonyesha, wala kumuchukia mutoto wa tumbo lake? Hata kama mama anaweza kumusahau mutoto wake, mimi sitakusahau hata kidogo.
Waadui wao wanavizia maisha yao watauzunguka muji ule kwa vita. Wataleta taabu na masumbuko hata watu watakula wenzao. Nitawafanya wakule miili ya wana na wabinti zao.
Macho yangu yamevimba kwa kulia, roho yangu imechafuka, moyo wangu una huzuni nyingi, kwa sababu ya kuangamizwa kwa watu wangu, kwa sababu watoto wachanga na wale wanaonyonya wanazimia katika barabara za muji.
Hukohuko katika muji wazazi watawakula watoto wao wenyewe na watoto watawakula wazazi wao. Nitatimiza hukumu zangu juu yenu na watakaobaki wazima nitawasambaza pande zote.