Namna gani muji uliokuwa mwaminifu sasa umegeuka kuwa kahaba! Wakati mumoja sheria ya Mungu ilifuatwa kabisa, haki ilikaa ndani yake. Sasa, ni muji wa wauaji.
Jinsi gani ulivyoporomoshwa toka mbinguni, wewe uliyekuwa nyota yenye kuangaza kwa mapambazuko. Jinsi gani ulivyoangushwa chini, wewe uliyeyashinda mataifa!
Usiku kucha uamukeamuke na kulia. Umufungulie Yawe yanayokuwa ndani ya moyo wako. Umwinulie mikono yako kwa kuwaombea watoto wako, watoto wanazimia na njaa popote katika barabara.
Kwa hiyo, anasema hivi: Muji wa Samaria nitaufanya kuwa mabomoko katika mbuga, shamba ambalo watu watapanda mizabibu. Mawe yaliyoujenga nitayatupa ndani ya bonde, na misingi yake nitaichimbuachimbua.