Lakini, ee Yawe wa majeshi, wewe unayehukumu kwa haki, unayechunguza mioyo na akili za watu, unijalie nione jinsi utakavyowalipiza kisasi, maana ninayaweka maneno yangu kwako.
Nami nikasema: Lakini wewe Yawe unanielewa vizuri; unikumbuke na kuja kunisaidia. Unilipizie watesaji wangu kisasi. Wewe ni muvumilivu, usiniache niangamie; kumbuka kwamba ninatukaniwa kwa ajili yako.
Kweli, mwangamizaji anashambulia Babeli; waaskari wake wametekwa, pinde zao zimevunjwavunjwa. Mimi Yawe ni Mungu mwenye kuazibu, hakika mimi nitalipiza kisasi kamili.
Mukimbie kutoka Babeli, kila mutu apate kuyaokoa maisha yake! Musiangamizwe katika azabu yake, maana huu ndio wakati wa Mungu wa kulipiza kisasi, anaiazibu Babeli kama inavyostahili.
Mutendee muji ule sawa vile ulivyowatendea. Mulipize matendo yake mara mbili zaidi. Na katika kile kikombe alimochanganya divai yake, mumuchangie divai inayokuwa kali mara mbili zaidi kuliko ile aliyowapa.
Watu wale wakalalamika hivi kwa sauti kubwa: “Bwana mutakatifu na mwenye ukweli, mpaka wakati gani utaendelea kungojea kuwahukumu wakaaji wa dunia na kuwaazibu kwa sababu ya kuuawa kwetu?”