na malaika ambaye aliniokoa katika mabaya yote, awabariki vijana hawa! Jina langu na majina ya babu zangu, Abrahamu na Isaka, yadumishwe katika vijana hawa; nao waongezeke kwa wingi katika dunia.”
Lakini, ee Yawe wa majeshi, wewe unayehukumu kwa haki, unayechunguza mioyo na akili za watu, unijalie nione jinsi utakavyowalipiza kisasi, maana ninayaweka maneno yangu kwako.
Lakini mimi, Mukombozi wao ni mwenye nguvu. Yawe wa majeshi ndilo jina langu. Hakika nitatetea maneno yao kusudi nilete amani katika inchi yao, lakini taabu kwa wakaaji wa Babeli.
Kwa hiyo Yawe anasema hivi: Nitawatetea juu ya maneno yenu, na kulipiza kisasi kwa ajili yenu. Nitaikausha bahari ya Babeli na kuvifanya visima vyake vikauke.
Daudi aliposikia kwamba Nabali amekufa, alisema: “Atukuzwe Yawe ambaye amemulipiza kisasi Nabali kwa kunitukana, naye Yawe ameniepusha mimi mutumishi wake kutenda maovu. Yawe amemwazibu Nabali kwa uovu wake.” Kisha Daudi alituma watu kwa kumuchumbilia Abigaili akuwe muke wake.