Sasa ninakuomba unisikilize, ee bwana wangu mufalme. Ninakusihi sana ulikubali ombi langu. Tafazali usinirudishe tena katika kifungo katika nyumba ya katibu Yonatani, nisipate kukufia humo.
Basi, wakamutwaa Yeremia wakamutia katika kisima cha Malkia mwana wa mufalme ambacho kilikuwa katika kiwanja cha walinzi. Walimushusha Yeremia ndani kwa kamba. Ndani ya kisima hicho hamukukuwa maji lakini matope, naye Yeremia akazama katika matope.
Bwana wangu mufalme, watu hawa wamefanya kitu kibaya. Wamemutia yule nabii Yeremia katika kisima ambamo kwa kweli atakufa kwa njaa, kwa maana hakuna chakula tena katika muji.
Halafu mufalme Dario akatoa amri, naye Danieli akaletwa na kutupwa katika pango la simba. Mufalme akamwambia Danieli: Mungu wako ambaye unamutumikia siku zote akuokoe.
Jiwe likaletwa na kuwekwa kwenye mulango wa lile pango. Mufalme akapiga muhuri wake mwenyewe na ule wa wakubwa wake, kusudi uamuzi uliotolewa juu ya Danieli usibadilishwe.