Maana Yawe atasimama kama kule kwenye mulima Perasimu; atawaka hasira kama kule katika bonde la Gebeoni. Atatimiza mupango wake wa ajabu; atatenda kazi yake ya ajabu sana.
Basi, uwaambie: Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– mimi sikifurahii kifo cha mutu mwovu, lakini ninapenda mutu mwovu aachane na mwenendo wake mubaya, apate kuishi. Mugeuke, muachane na mwenendo wenu mubaya, enyi Waisraeli! Kwa nini munataka kufa?