Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Maombolezo 3:31 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

31 Yawe hatatutupilia milele.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Maombolezo 3:31
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sisi wote tutakufa. Sisi ni kama maji yaliyomwangika chini ambayo hayawezi kuzoleka. Lakini Mungu hataki Abusaloma akufe sasa au aendelee kuishi mbali naye.


Kutokana na hayo, nitawaazibu wazao wa Daudi, lakini si siku zote.’ ”


Usiku ninawazawaza; moyo wangu unafikiri, nayo roho yangu inajiuliza:


Yawe hatawaachilia watu wake; hatawatupa hao wanaokuwa mali yake.


Aliwaazibu watu wake kwa kuwapeleka katika uhamisho. Wakati wa upepo mukali wa mashariki, aliwaondoa kwa pigo kali.


Maana sitaendelea kugombana wala kuwakasirikia siku zote, maana hao niliowaumba watazimia mbele yangu, nami ndiye niliyewapa pumzi yangu ya uzima.


Yawe anasema hivi: Kama mbingu zinaweza kupimwa, na misingi ya dunia kuchunguzwa, basi, nitawatupilia wazao wa Israeli, kwa sababu ya mambo yote waliyotenda.


Nitafanya nao agano la milele, kwamba sitaacha kuwatendea mema hata kidogo; nitaweka ndani ya mioyo yao utii kwa ajili yangu kusudi wasiniache tena.


Haujasikia namna watu hawa wanavyosema, kwamba mimi Yawe nimewatupilia mbali watu wa Israeli na watu wa Yuda, jamaa mbili nilizochagua? Wamewazarau watu wangu, hata kuwaona kwamba wao si taifa.


Ee Mungu, ni nani anayekuwa kama wewe? Wewe unasemehe zambi za watu wako waliobaki, wala hauyaangalii makosa yao. Hasira yako haidumu milele, lakini unapendelea zaidi kutuonyesha wema wako.


Yawe anasema hivi: Ingawa Waasuria ni wengi na wenye nguvu, wao wataangushwa na kuangamizwa. Ingawa nimewatesa ninyi watu wangu, sitawatesa tena zaidi.


Kwa heshima ya jina lake kubwa, Yawe hatawatupa watu wake kwa sababu amependa kuwafanya ninyi mukuwe watu wake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ