3 Amenyoosha mukono wake juu yangu mimi tu, akiniazibu tena na tena muchana kutwa.
Nilikuwa nimestarehe, lakini akanivunjavunja. Alinikamatia katika shingo na kunipasua vipandevipande. Akanifanya shabaha ya mishale yake,
Munionee huruma, munionee huruma, enyi warafiki zangu; maana mukono wa Mungu umenigusa.
Kama nimekunjia yatima ngumi katika tribinali nikijua nitapendelewa na waamuzi,
Mishale ya Mungu Mwenye Uwezo imenichoma; nafsi yangu imekunywa sumu yake. Vitisho vya Mungu vimenipata.
Ee Yawe, usiniazibu kwa hasira yako, usiniadibishe kwa kasirani yako.
Nitapigana nawe; nitayeyusha uchafu wako kabisa, na kuondoa takataka yako yote.
Kwa hiyo hasira ya Yawe iliwawakia watu wake, akaunyoosha mukono wake juu yao, akawaazibu. Milima ikatetemeka, maiti zao zikakuwa kama takataka katika barabara za muji. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.
Lakini wao waliasi, wakaihuzunisha roho yake takatifu. Basi, Mungu akageuka, akakuwa adui yao; yeye mwenyewe akapigana nao.
Yawe atamutenga kutoka kati ya makabila yote ya Israeli apatwe na hasara kufuatana na laana zote za agano zilizoandikwa katika kitabu hiki.