Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Maombolezo 3:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Ni vizuri kwa mutu kungojea kwa utulivu wokovu unaotoka kwa Yawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Maombolezo 3:26
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hamutahitaji kupigana vita hivi. Ninyi mujipange tu halafu mungojee, na mutaona Yawe akiwashinda kwa jina lenu. Enyi watu wa Yuda na Yerusalema, musiogope wala musifazaike. Muende kwa vita, naye Yawe atakuwa pamoja nanyi!”


Ee Yawe, ninakungojea uniokoe; mimi ninatimiza amri zako.


Ninatamani sana uniokoe, ee Yawe; sheria yako ndiyo furaha yangu.


Ninamutumainia Yawe kwa moyo wangu wote. Ninaaminia sana neno lake.


Umutumainie Yawe na kushika njia yake, naye atakuinua uirizi inchi, na kuwaona waovu wakiongolewa.


Tulia mbele ya Yawe, umungojee kwa uvumilivu; usihangaike juu ya wale wanaofanikiwa, ndio watu wanaojaliwa katika mipango yao mibaya.


“Muangalie yaliyomupata mutu huyu! Yeye hakutaka Mungu akuwe kimbilio lake, lakini alitegemea wingi wa mali yake, na kutafuta humo usalama wake!”


Ninajua Mungu ni musaada wangu, Yawe anaimarisha maisha yangu.


Kwa Mungu peke yake ninapata utulivu, wokovu wangu unatoka kwake.


Lakini, kwangu ni vizuri kuwa karibu na Mungu. Wewe Bwana wangu Yawe ndiwe usalama wangu. Nitatangaza mambo yote uliyotenda!


Musa akawaambia Waisraeli: “Musiogope! Musimame imara! Leo mutaona jinsi Yawe atakavyowaokoa. Maana, hawa Wamisri munaowaona leo, hamutawaona tena.


Yawe atawapigania. Ninyi mutakaa kimya tu.”


Bwana wetu Yawe, Mutakatifu wa Israeli anasema hivi: Mukinirudilia na kutulia mutaokolewa; kwa utulivu na kunitumainia mutapata nguvu. Lakini ninyi hamukutaka.


Maana musaada wa Misri ni bure, haufai kitu; kwa hiyo nimeipanga Misri jina: Nyoka mukubwa asiyekuwa na nguvu!


Umwambie akuwe macho, atulie na asiogope wala asivunjike moyo, kwa sababu ya hasira kali ya mufalme Resini wa Aramu, na ya mwana wa Remalia. Hao wawili ni kama tu moshi wa kuni zinazozimika.


Katikati ya miungu ya uongo ya mataifa nani anayeweza kunyesha mvua? Au, ni mbingu ndiyo inaweza kutoa manyunyu? Si ni wewe ee Yawe, Mungu wetu? Tunakuwekea wewe tumaini letu, maana ni wewe unayefanya haya yote.


Ni vizuri kwa mutu kujifunza uvumilivu tangu wakati wa ujana wake.


Maono haya yanangoja wakati uliopangwa; ni maono ya ukweli juu ya mwisho. Kama yanaonekana kuchelewa, uyangojee; hakika yatafika, wala hayatachelewa.


Ni vizuri kushugulika na mambo mema siku zote, wala si wakati ninapokuwa pamoja nanyi tu.


Basi musikate tumaini, kwa maana litawaletea zawadi kubwa.


Kwa maana sisi wote tunaishi katika ushirika na Kristo ikiwa tunachunga mpaka mwisho lile tumaini tulilopata kwa mwanzo.


Kwa sababu hiyo, mukuwe tayari kwa kutumikisha akili yenu. Mukeshe na muweke tumaini lenu lote katika baraka ile mutakayopewa wakati Yesu atakapotokea.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ