Kwa hiyo Yawe akaniambia: Wewe mwanadamu! Mifupa hiyo ni mufano wa watu wote wa inchi ya Israeli. Wao, wanasema: Mifupa yetu imekauka, matumaini yetu yamepotea nasi tumekwisha kabisa.
Daudi akajisemesha ndani ya moyo: “Siku moja, Saulo ataniangamiza. Jambo zuri kwangu ni kukimbilia katika inchi ya Wafilistini. Saulo atakata tamaa kunitafuta ndani ya mipaka ya inchi ya Israeli, nami nitakuwa salama kutoka katika mikono yake.”