Kwa hiyo, Yawe wa majeshi anasema hivi juu ya manabii wa Yerusalema: Nitawakulisha uchungu, na kuwapa maji yenye sumu wakunywe. Maana kutoka kwa manabii wa Yerusalema kutomwogopa Mungu kumeenea kila pahali katika inchi.
Yawe akaniamuru: Utawaambia kwamba: Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Mukunywe, mulewe na kutapika; muanguke wala musisimame tena, kwa sababu ya mauaji nitakayosababisha kati yenu.
Wewe Yuda, hayo yote yamekupata kwa ajili ya mwenendo na matendo yako. Hiyo ndiyo hasara inayokufikia, tena ni yenye uchungu; yamepenya mpaka ndani ya moyo wako.
Nitawatawanya kati ya mataifa ambayo wao wenyewe wala babu zao hawakupata kuyajua; na kisha nitatuma vita nyuma yao mpaka hapo nitakapowaangamiza wote.