Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Maombolezo 2:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Yawe amekuwa kama adui, ameangamiza watu wa Israeli; ameharibu nyumba zake kubwa zote, amevibomoa vikingio vyake. Amewazidishia watu wa Yuda kilio na maombolezo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Maombolezo 2:5
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Akaichoma kwa moto nyumba ya Yawe, nyumba ya kifalme na nyumba zote za Yerusalema; kila nyumba kubwa akaichoma kwa moto.


Mbona unageuza uso wako mbali nami? Kwa nini unanitendea kama adui yako?


Ameichochea kasirani yake juu yangu; ameniona kuwa kama adui yake.


Umefuta agano ulilofanya na mutumishi wako; umeitupa taji yake ya kifalme ndani ya mavumbi.


Umebomoa kuta zote za muji wake; umezivunjavunja nafasi zake za kukimbilia.


lakini mimi Mungu nitahuzunisha Yerusalema, ndani yake kutakuwa vilio na maombolezo, muji wenyewe utakuwa kama mazabahu.


Lakini wao waliasi, wakaihuzunisha roho yake takatifu. Basi, Mungu akageuka, akakuwa adui yao; yeye mwenyewe akapigana nao.


Kisha Yawe akaniambia: Hata kama Musa na Samweli wangesimama mbele yangu na kunisihi, singewahurumia watu hawa. Uwaondoe kabisa mbele yangu. Uwaache waende!


Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Zedekia, nitakugeuzia wewe mwenyewe silaha unazozitumia kwa kupigana na mufalme wa Babeli na waaskari wake wanaozunguka inje ya kuta za muji wenu. Nitazikusanya silaha zile katikati ya muji huu.


Wapenzi wako wote wamekusahau; hawajali kitu chochote juu yako. Nimekupiga sawa vile ungekuwa adui yangu. Umeazibiwa bila huruma, kwa sababu kosa lako ni kubwa, zambi zako ni nyingi sana.


Aliteketeza kwa moto nyumba ya Yawe, nyumba ya kifalme na nyumba zote za Yerusalema; kila nyumba kubwa ilichomwa kwa moto.


Yawe ameharibu bila huruma makao yote ya wazao wa Yakobo. Kwa kasirani yake amevibomoa vikingio vya watu wa Yuda. Ametupa chini na kuchafua ufalme wao na watawala wake.


Amevuta upinde wake kama adui, na kuuweka mukono wake wa kuume tayari, amewaua wote waliopendeza macho. Amemwanga hasira yake kama moto katika hema yetu watu wa Sayuni.


Basi akakikunjua mbele yangu, nacho kilikuwa kimeandikwa mbele na nyuma maneno ya maombolezo, kilio na hasara.


Samweli akasema: “Kwa nini unaniomba shauri ikiwa Yawe amekuachilia na amekuwa adui yako?


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ