Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Maombolezo 1:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Watu wa Yuda wamekwenda katika uhamisho, wakijaa mateso na kuwa katika utumwa mukali. Wanakaa kati ya watu wa mataifa, wala hawapati nafasi ya kupumzikia. Waliowafuatilia wamewakamata wakiwa katika taabu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Maombolezo 1:3
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nebuzaradani, mukubwa wa waaskari wa mufalme, akawapeleka katika uhamisho watu waliokuwa wamebakia katika muji na wale wote waliokuwa wamejitoa wenyewe kwa mufalme wa Babeli pamoja na watu wengine wote.


Mufalme Nebukadneza wa Babeli akawapiga na kuwaua watu hao kule Ribla katika inchi ya Hamati. Hivyo watu wa Yuda wakapelekwa kuwa watumwa inje ya inchi yao.


Basi, sehemu ya ukuta wa muji ukabomolewa, naye mufalme pamoja na waaskari wote wakakimbia wakati wa usiku wakipitia katika bustani ya mufalme kwenye mulango katikati ya kuta mbili, wakaenda upande wa Araba, ingawa Wababeli walikuwa wameuzunguka muji.


Lakini waaskari wa Babeli wakamufuata mufalme na kumuteka kwenye bonde za Yeriko, nao waaskari wake wote wakamwacha, wakatawanyika.


Miji ya Negebu imezungukwa kwa vita; hakuna anayeweza kuingia ndani yao. Watu wa Yuda wamekamatwa mateka, wote kabisa wamepelekwa katika utumwa.


Nitaita wavuvi wengi kuja kuwanasa watu hawa. Kisha, nitaita wawindaji wengi kuja kuwawinda juu ya kila mulima, kila kilima na katika mapango ya chini ya mawe.


Nitawafanya kuwa kitu cha kuchukiza mbele ya falme zote za dunia. Watakuwa kitu cha zihaka, kitu cha kuzomewa, kuchekelewa na kulaaniwa kila fasi nitakapowasambaza.


Kisha, Nebuzaradani, mukubwa wa walinzi wa mufalme, aliwapeleka katika uhamisho kule Babeli watu waliokuwa wamebaki katika muji na wale waliokuwa wamejitoa kwake pamoja na wafundi wote waliokuwa wamebaki.


Nebuzaradani mukubwa wa waaskari wa mufalme, aliwapeleka katika uhamisho watu waliokuwa wamebakia katika muji na wale waliojitoa wenyewe kwa mufalme wa Babeli pamoja na wafundi.


Lakini kundi la Wakaldea lilimufuatilia mufalme na kumukamata katika bonde la Yeriko, waaskari wake wote wakatawanyika na kumwacha.


Milango yake imezama ndani ya udongo, ameharibu na kuvunjavunja vifungio vyake. Mufalme na wakubwa wake wako katika uhamisho kati ya mataifa. Hakuna sheria tena, manabii wake hawapati tena maono kutoka kwa Yawe.


Watu waliwapigia kelele wakisema: Mutoke, enyi munaokuwa wachafu! Mutoke! Mutoke! Musiguse kitu chochote. Hivyo wakakuwa wakimbizi na kutangatanga; watu wa mataifa walisema: Hawa hawatakaribishwa kukaa kwetu!


Tunalazimishwa kufanya kazi kama punda, tumechoka, lakini haturuhusiwi kupumzika.


Sehemu moja ya tatu ya watu wako, ee Yerusalema, itakufa kwa ugonjwa mukali na kwa njaa. Sehemu ingine moja ya tatu itakufa katika vita. Na sehemu moja ya tatu inayobaki nitaisambaza pande zote za dunia na nitachomoa upanga wangu na kuwafuatilia nyuma.


Kwa hiyo mutawatumikia waadui zenu ambao Yawe atawatuma mbele yenu, kwa njaa, kiu na uchi, na ukosefu wa kila kitu. Atawafunga nira ya chuma mpaka awaangamize.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ