Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Maombolezo 1:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Sikiliza ninavyolalamika; hakuna wa kunifariji. Waadui zangu wote wamesikia juu ya taabu yangu: wanafurahi kwamba umeniletea hasara. Uifanye ile siku uliyoahidi ifike, uwafanye nao wateseke kama mimi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Maombolezo 1:21
37 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini mimi nilipoanguka, walikusanyika kunisimanga. Walikusanyika kuniuzi. Wageni nisiowajua walinizomea bila kukoma, wala hakuna aliyewazuia.


Lakini Yawe anamuchekelea mwovu, kwa maana anajua mwisho wake ni karibu.


Lakini ninakutumainia wewe, ee Yawe; wewe, ee Yawe, Mungu wangu, ndiwe utakayenijibu.


Yawe amelivunja gongo la waovu, ameivunja fimbo ya kifalme ya watawala,


ambayo walipiga nayo watu kwa hasira bila kukoma, na kuwatawala kwa kuwatesa bila huruma.


Lakini wote wanaokuangamiza, wataangamizwa vilevile, na waadui zako wote watapelekwa katika uhamisho; nao wanaokukamata mateka watakamatwa mateka, nao wanaokuwinda, nitawawinda.


Ee Moabu, si ulimuchekelea Israeli! Ulimuhesabu kama mwenzake na wanyanganyi hata ukakuwa unatikisa kichwa chako kila mara uliposema juu yake.


Enyi wanyanganyi wa mali yangu, ijapokuwa munafurahi na kushangilia, munarukaruka kama mwana-ngombe anayepepeta ngano, na kulia kama farasi dume,


Mupigie kelele za vita pande zote; sasa Babeli umejitoa ukamatwe. Vikingio vyote vimeanguka, kuta zake zimebomolewa. Ni malipizi ya Yawe. Basi muulipize kisasi. Muutendee kama vile ulivyotendea wengine.


Muwaite wapiga mishale waishambulie Babeli. Mupeleke kila mutu anayejua kuvuta upinde. Muuzunguke muji kusikuwe mutu yeyote atakayetoroka. Muulipize kadiri ya matendo yake yote; muutendee kama ulivyowatendea wengine, maana kwa kiburi ulinizarau mimi Yawe, Mutakatifu wa Israeli.


Mimi, ninapigana nawe, ewe mwenye kiburi. –Ni ujumbe wa Bwana wa wote, Yawe wa majeshi.– Maana siku yako ya azabu imefika, wakati nitakapokuazibu umetimia.


Nitaiazibu Babeli na wakaaji wote wa Kaldea mukiona kwa macho yenu wenyewe, kwa sababu ya uovu wote walioufanya katika Sayuni. –Ni ujumbe wa Yawe.


Babeli umesababisha vifo katika dunia yote; sasa muji wenyewe utaangamizwa kwa ajili ya mauaji ya Waisraeli.


Kwa sababu ya hayo ninalia, machozi yananitiririka, sina mutu yeyote wa kunifariji; hakuna yeyote wa kunitia moyo. Watoto wangu wameachwa ukiwa, maana adui yangu amenishinda.


Unalia usiku kucha; machozi yanatiririka juu ya mashavu yake. Hakuna hata mumoja kati ya wapenzi wake kwa kuufariji. Rafiki zake wote wameudanganya; wamekuwa waadui zake.


Uwaazibu kwa ajili ya uovu wao wote. Uwatendee kama ulivyonitendea mimi, kwa sababu ya makosa yangu yote. Ninaugua sana kwa maumivu na moyo wangu unazimia.


Barabara za Sayuni zinaomboleza, maana hakuna anayepita kwa sikukuu. Milango yake yote ni tupu, makuhani wake wanaugua, wabinti zake wana huzuni, na muji wenyewe uko katika uchungu.


Muji Yerusalema ulitenda zambi kubwa, ukakuwa muchafu kwa ajili ya zambi zake. Wote waliousifia wanauzarau, maana wameuona uchi wake. Muji wenyewe unaugua na kujificha kwa ajili ya haya.


Wapita njia wote wanakuchekelea; wanakupigia muunzi, ee Yerusalema, wakitikisa vichwa vyao kwa mazarau na kusema: Huu ndio ule muji uliofikia ukamilifu wa uzuri, muji uliokuwa furaha ya dunia nzima?


Waadui zako wote wanakuzomea, wanakupigia muunzi na kukusagia meno, nao wanasema: Tumemwangamiza! Kweli, siku ile tuliyoingojea kwa hamu sasa imefika na tumeiona!


Wewe mwanadamu! Watu wa muji wa Tiro wameuchekelea Yerusalema na kusema: Aha! Yerusalema muji ambao watu wote walipitia, umeangamizwa! Sasa umetuachia nafasi; utajiri wake umeharibika!


Mutendee muji ule sawa vile ulivyowatendea. Mulipize matendo yake mara mbili zaidi. Na katika kile kikombe alimochanganya divai yake, mumuchangie divai inayokuwa kali mara mbili zaidi kuliko ile aliyowapa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ