Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Maombolezo 1:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Ona, ee Yawe, ninavyokuwa tabani. Roho yangu imechafuka, moyo wangu unaugua maana nimekuasi vibaya. Kule inje kumejaa mauaji, ndani nako ni kama kifo tu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Maombolezo 1:20
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Moyo wangu unahangaika wala hautulii hata kidogo. Siku za mateso zimenipata.


Atashangilia mbele ya watu na kusema: “Nilitenda zambi na kupotosha usawa, nami sikuazibiwa kutokana na hayo.


Wanafungua vinywa vyao kama simba, tayari kushambulia na kurarua.


Viungo vyangu vimeshambuliwa na homa; hakuna uzima katika mwili wangu.


Anayeficha makosa yake hatafanikiwa, lakini anayeungama na kuyaacha atahurumiwa.


Hivyo, nafsi yangu inalilia Moabu kama kinubi, na moyo wangu kwa ajili ya muji wa Kiri-Heresi.


Ninalia kama mbaruwayi, ninaugua kama njiwa. Macho yangu yamefifia kwa kuangalia juu. Ee Bwana, ninateseka; ukuwe wewe usalama wangu!


Nikienda inje katika mbuga, ninaiona maiti ya waliouawa kwa vita; nikiingia ndani katika muji, ninaona tu maiti ya waliokufa kwa njaa! Manabii na makuhani wanashugulikia mambo yao katika inchi, lakini hawajui wanalofanya.


Tunakubali uovu wetu, ee Yawe, tunakubali uovu wa babu zetu, maana, tumekukosea wewe.


wewe unasema: Mimi sina kosa; hakika hasira yake imegeuka mbali nami. Lakini mimi nitakuhukumu kwa sababu unasema kwamba haukutenda zambi.


Wewe, kubali tu kosa lako: kwamba umeniasi mimi Yawe, Mungu wako; kwamba chini ya kila muti wenye majani, umeonyesha mapenzi yako kwa miungu mingine, wala haukuitii sauti yangu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Efuraimu ni mwana wangu mupendwa; yeye ni mutoto wangu ninayemupenda sana. Ndiyo maana kila mara ninapomutisha, ninaendelea kumukumbuka. Moyo wangu unamwelekea kwa wema; hakika nitamuhurumia. –Ni ujumbe wa Yawe.


Uchungu, uchungu! Ninagaagaa kwa uchungu! Moyo wangu unapigapiga vibaya. Wala siwezi kukaa kimya. Maana ninaogopa mulio wa baragumu, ninasikia kelele la vita.


Kwa hiyo, moyo wangu unaomboleza juu ya watu wa Moabu na watu wa Kiri-Heresi, kama vile filimbi; maana hata mali yote waliyojipatia imeangamia.


Watu wa Yerusalema wote wanaugua, wakitafuta chakula; wanatoa vitu vyao vya bei kali kwa kupata chakula, kusudi wajirudishie nguvu zao. Nao muji unalia, Ee Yawe, uniangalie, ona jinsi nilivyogeuka kuwa zaifu.


Lakini Yawe amefanya sawa kwa maana nimeliasi neno lake. Munisikilize enyi watu wote, muyaangalie mateso yangu. Wabinti zangu na vijana wangu wanaume wamepelekwa katika utumwa.


Muji Yerusalema ulitenda zambi kubwa, ukakuwa muchafu kwa ajili ya zambi zake. Wote waliousifia wanauzarau, maana wameuona uchi wake. Muji wenyewe unaugua na kujificha kwa ajili ya haya.


Uchafu wake ulionekana waziwazi, lakini muji wenyewe haukujali mwisho wake. Anguko lake lilikuwa kubwa sana; hakuna anayeweza kuufariji. Unasema: Angalia, ee Yawe, mateso yangu, maana adui yangu ameshinda.


Macho yangu yamevimba kwa kulia, roho yangu imechafuka, moyo wangu una huzuni nyingi, kwa sababu ya kuangamizwa kwa watu wangu, kwa sababu watoto wachanga na wale wanaonyonya wanazimia katika barabara za muji.


Taji tuliojivunia imeanguka. Ole kwetu maana tumetenda zambi!


Inje kuna kifo kwa upanga na ndani ya muji kuna ugonjwa mukali na njaa. Wanaokuwa katika vijiji watakufa kwa upanga; wanaokuwa katika muji wataangamizwa na njaa na ugonjwa mukali.


Tumetenda zambi, tumekosa, tumetenda maovu na kukuasi. Tumevunja amri zako na maagizo yako.


Ewe Efuraimu, ninaweza kukuacha namna gani? Ninaweza kukutupilia, ewe Israeli namna gani? Nitaweza namna gani kukufanya kama muji wa Adama? Nitaweza namna gani kukutendea kama Zeboimu! Ninazuizwa na moyo wangu; huruma yangu imezidi kuwa motomoto.


Nikasikia hayo, matumbotumbo yangu yakatetemeka. Midomo yangu inatetemeka kwa hofu, mifupa yangu inateguka, miguu yangu inatetemeka. Ninangojea kwa utulivu siku ile ya hasara, ambayo inawafikia wale wanaotushambulia.


Vita itasababisha vifo vingi inje, na ndani ya nyumba hofu itawatawala. Vijana wanaume na wanawake watauawa, hata wenye kunyonya na wazee wenye imvi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ