Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Maombolezo 1:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Ninainyoosha mikono yangu lakini hakuna wa kunifariji. Yawe ametoa amri juu yangu mimi Yakobo, wajirani zangu wakuwe waadui zangu. Kweli, mimi Yerusalema nimekuwa kitu kichafu kwao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Maombolezo 1:17
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha Solomono alisimama kwenye mazabahu ya Yawe, mbele ya Waisraeli wote, aliinua mikono yake juu,


tafazali, chochote ambacho mutu yeyote au watu wako wote wa Waisraeli wanakuomba na kukusihi, kila mutu akijua taabu ndani ya moyo wake na kunyoosha mikono yake kuelekea nyumba hii,


Katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, mwaka wa tisa wa utawala wa Zedekia, Nebukadneza mufalme wa Babeli akafika na waaskari wake kwa kushambulia Yerusalema. Akapiga kambi mbele ya muji ule na kujenga ngazi kuuzunguka.


Kisha nikaona mateso yote yanayofanyika chini ya jua. Watu wanaogandamizwa wanalia machozi, lakini hakuna mutu yeyote anayewafariji. Wagandamizaji wao wana nguvu, ndiyo sababu hakuna wa kuwafariji.


Munapoinua mikono yenu kwa kuomba, nitauficha uso wangu nisiwaone. Hata mukiomba sana sitawasikia, maana mikono yenu imejaa damu.


Ewe Yerusalema, uliteseka, ulitaabishwa na kukosa wa kukufariji, lakini nitakujenga upya kwa mawe ya bei kali, misingi yako itakuwa ya mawe ya yakuti.


Urizi wangu umekuwa kama ndege muzuri ambaye anashambuliwa pande zote na ndege wakali? Muende kuwakusanya nyama wote wa pori, muwalete wakule.


Ni nani atakayewahurumia, enyi watu wa Yerusalema? Ni nani atakayeomboleza juu yenu? Nani atasimama kuuliza habari zenu?


Wote, wakubwa kama vile wadogo, watakufa katika inchi hii; nao hawatazikwa, wala hakuna atakayeomboleza juu yao. Hakuna atakayejikatakata wala kunyolewa upaa kwa ajili ya kifo chao.


Nitawaamuru nao wataurudia katika muji huu. Wataushambulia, watauteka na kuuteketeza kwa moto. Nitaifanya miji ya inchi ya Yuda kuwa ukiwa bila wakaaji. –Ni ujumbe wa Yawe.


Nilisikia sauti kama ya mwanamuke anayezaa, malalamiko kama ya mwenye kuzaa mutoto wa kwanza. Ilikuwa sauti ya Yerusalema akipumuapumua kwa uchungu, na kuinyooshanyoosha mikono yake, akisema: Ole wangu! Wanakuja kuniua!


Watu wataufikia kama vile wachungaji na makundi yao, watasimamisha hema zao kandokando yake, kila wamoja upande wao kwa kulisha makundi yao.


Huzuni yangu haiwezi kutulizwa, moyo wangu unaugua ndani yangu.


Kwa sababu ya hayo ninalia, machozi yananitiririka, sina mutu yeyote wa kunifariji; hakuna yeyote wa kunitia moyo. Watoto wangu wameachwa ukiwa, maana adui yangu amenishinda.


Niliwaita wapenzi wangu, lakini wao wakanidanganya. Makuhani na wazee wangu wamekufia katika muji, wakijitafutia chakula kusudi wajirudishie nguvu zao.


Unalia usiku kucha; machozi yanatiririka juu ya mashavu yake. Hakuna hata mumoja kati ya wapenzi wake kwa kuufariji. Rafiki zake wote wameudanganya; wamekuwa waadui zake.


Sikiliza ninavyolalamika; hakuna wa kunifariji. Waadui zangu wote wamesikia juu ya taabu yangu: wanafurahi kwamba umeniletea hasara. Uifanye ile siku uliyoahidi ifike, uwafanye nao wateseke kama mimi.


Muji Yerusalema ulitenda zambi kubwa, ukakuwa muchafu kwa ajili ya zambi zake. Wote waliousifia wanauzarau, maana wameuona uchi wake. Muji wenyewe unaugua na kujificha kwa ajili ya haya.


Uchafu wake ulionekana waziwazi, lakini muji wenyewe haukujali mwisho wake. Anguko lake lilikuwa kubwa sana; hakuna anayeweza kuufariji. Unasema: Angalia, ee Yawe, mateso yangu, maana adui yangu ameshinda.


Watu waliwapigia kelele wakisema: Mutoke, enyi munaokuwa wachafu! Mutoke! Mutoke! Musiguse kitu chochote. Hivyo wakakuwa wakimbizi na kutangatanga; watu wa mataifa walisema: Hawa hawatakaribishwa kukaa kwetu!


Wewe mwanadamu! Waisraeli walipoishi katika inchi yao waliichafua kwa mienendo na matendo yao. Niliyaona matendo yao kuwa sawa na mwanamuke anayekuwa muchafu wakati wa ugonjwa wake wa mwezi.


Waisraeli wamemezwa, wanakuwa kati ya mataifa mengine, kama chombo kisichokuwa na faida yoyote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ