Maombolezo 1:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
15 Yawe aliwakataa waaskari walionilinda, alitangaza wakati kamili wa kuniazibu kuwaponda vijana wangu wanaume. Aliwaponda kama katika kikamulio, watu wangu wa Yuda.
naye Yehu akawaambia: “Mumutupe chini!” Wakamutupa chini na damu yake ikasambaa juu ya ukuta na kwenye farasi. Yehu akapitisha farasi na gari lake juu ya maiti yake
Ni nani aliyemwita shujaa toka mashariki, mutu ambaye anapata ushindi popote anapoenda? Mimi ninayaweka mataifa katika mikono yake, naye anawaponda wafalme chini ya miguu yake! Upanga wake unawafanya kuwa kama mavumbi, kwa upinde wake anawapeperusha kama maganda.
Na sasa nitawaambia jinsi nitakavyolifanya hilo shamba langu. Nitaubomoa upango wake, nalo litaharibiwa. Nitaubomoa ukuta wake, nalo litakanyagwakanyagwa.
Kwa hiyo uwaache watoto wao wakufe kwa njaa, uwaache wakufe kwa vita. Wake zao wakuwe tasa na wajane. Waume zao wakufe kwa magonjwa makali na vijana wao wachinjwe kwa upanga katika vita.
Hata kama mukiwashinda waaskari wote wa Wakaldea wanaopigana nanyi na kunabaki tu katika mahema yao wale walioumizwa, hao watasimama na kuuteketeza muji huu kwa moto.
Mukuje kumushambulia kutoka kila upande; muzifungue gala zake za chakula; mumulundikie malundo ya ngano! Muiangamize kabisa inchi hii; musiache kitu chochote!
Mufalme Nebukadneza wa Babeli aliuharibu na kuuponda Yerusalema aliuacha kama chungu kitupu; aliumeza kama vile nyoka mukubwa. Alijaza tumbo lake vitu vyake vizurivizuri, akautupilia mbali kama matapiko.
Nimejaa hasira ya Yawe nami ninachoka kwa kuizuia. Kwa hiyo Yawe akaniambia: Umwange hasira ile katika barabara juu ya watoto na vilevile juu ya makundi ya vijana; nayo itawaangukia wote, mume na muke, nao wazee na hata wale ambao wamezeeka sana.
Maiti za vijana na wazee zimelala ndani ya mavumbi katika barabara, wabinti na vijana wangu wameuawa kwa upanga; umewaua bila huruma siku ya hasira yako.
Halafu adui yangu ataona hayo naye atafunikwa na haya; maana aliniambia: Basi Yawe, Mungu wako, yuko wapi? Mimi mwenyewe nitamwona adui akianguka; atakanyagwakanyagwa chini kama matope katika njia.
Wamoja watauawa kwa vita na watapelekwa kuwa wafungwa katika inchi za mataifa yote. Vilevile mataifa mengine yatautawala Yerusalema mpaka nyakati zao za kuutawala zitakapokwisha.”
Basi munazania itakuwa namna gani? Hataazibiwa vikali zaidi yule anayemuzarau Mwana wa Mungu na kuihesabu kuwa bure damu ya agano la Mungu iliyomutakasa na kumutukana Roho wa neema?
Ndani ya kinywa chake mulitoka upanga mukali kwa kushinda mataifa. Naye atatawala kwa fimbo ya chuma na kukamua zabibu ndani ya kikamulio cha divai kinachojaa kasirani kali ya Mungu Mwenye Uwezo.