Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Maombolezo 1:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Namna gani muji uliokuwa umejaa watu, sasa unakaa peke yake! Ulikuwa na utukufu kati ya mataifa, sasa umekuwa kama mama mujane. Ulikuwa kama binti wa mufalme kati ya miji, sasa umekuwa mutumwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Maombolezo 1:1
38 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kusudi asiendelee kutawala akiwa kule Yerusalema, Neko mufalme wa Misri alimufunga kule Ribla katika inchi ya Hamati, akawalipisha watu wa Yuda kodi ya kilo elfu tatu na mia ine za feza na kilo makumi tatu na ine za zahabu.


Mufalme Yoyakimu akamupa Mufalme wa Misri feza na zahabu, lakini akailipisha inchi kodi kusudi aweze kutimiza mapenzi ya Mufalme wa Misri ya kupewa feza. Akawalipisha wanainchi feza na zahabu. Kila mumoja alitoa kufuatana na kiasi mufalme alichoamuru, naye akamupa Neko mufalme wa Misri.


Aliwatawala wafalme wote waliokuwa kuanzia muto Furati, mpaka inchi ya Wafilistini na mpaka kwenye mupaka na Misri.


Wafalme wenye nguvu wamepata kuutawala muji ule pamoja na jimbo la upande wa magaribi wa Furati wakilipisha kodi, malipo ya kuvuka mipaka na mengine.


Tena kukakuwa hata wale, waliolalamika, wakisema: “Kwa kulipa kodi ya mufalme juu ya mashamba na mizabibu yetu, tulipaswa kukopesha feza.


Kwa sababu ya zambi zetu, utajiri wa inchi hii unawaendea wafalme uliowaleta kwa kututawala. Wanatutawala jinsi wanavyopenda hata na nyama wetu wa ufugo wanawatendea jinsi wanavyopenda, tuko katika taabu kubwa sana.


Humo ndimo makabila yanamofika, ndiyo, makabila ya Yawe, kwa kumushukuru Yawe kama Waisraeli walivyoagiza.


Jinsi gani ulivyoporomoshwa toka mbinguni, wewe uliyekuwa nyota yenye kuangaza kwa mapambazuko. Jinsi gani ulivyoangushwa chini, wewe uliyeyashinda mataifa!


Kwa nini munapiga kelele za shangwe, na muji wote umechangamuka na kujaa vigelegele? Watu wenu waliokufa hawakuuawa katika vita, wala hawakuuawa katika mapigano.


Halafu watu watalia na kuomboleza kwenye milango ya muji; nao wataikaa ndani ya mavumbi katika ukiwa.


Kwa hiyo utajiuliza mwenyewe: Nani aliyenizalia watoto hawa wote? Nilikufiwa na watoto bila kupata wengine. Nilipelekwa katika uhamisho na kutupwa mbali; nani basi aliyewalea watoto hawa? Mimi niliachwa peke yangu, sasa, hawa wametoka wapi?


Bwana wetu Yawe amenifanya kuwa musikilivu, nami sikukataa wala kurudia nyuma.


Ujikungute mavumbi, usimame, ewe Yerusalema uliyekuwa mufungwa! Ujifungue minyororo yako katika shingo, ewe binti Sayuni uliyekamatwa mateka.


Ni furaha kabisa! Mujumbe anatokea kwenye mulima. Anatangaza habari njema za amani, heri, na ukombozi. Anauambia Sayuni: Mungu wako anatawala!


Usiogope, hautapata haya tena. Usifazaike, hautazarauliwa tena. Utaisahau haya uliyopata katika ujana wako, wala hautakumbuka tena mazarau ya ujane wako.


Maana Yawe anasema hivi: Mushangilie kwa furaha kwa ajili ya Yakobo, mupige vigelegele kwa ajili ya taifa kubwa, mutangaze, musifu na kusema: Yawe ameokoa watu wake, ameleta ukombozi kwa wale waliobaki kati ya Waisraeli!


Gedalia aliapa mbele yao na mbele ya waaskari wao akisema: Musiogope kuwatumikia Wakaldea. Mukae katika inchi mumutumikie mufalme wa Babeli, na mambo yote yatawaendekea vema.


wakamwendea Yeremia, wakamwambia: Tafazali sikiliza maombi yetu na kutuombea kwa Yawe, Mungu wako, sisi wote tuliobaki, kwa maana tulikuwa wengi, lakini sasa tumebaki wachache tu, kama unavyoona.


Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli anasema hivi: Ninyi mumeona hasara yote niliyouletea Yerusalema na miji yote ya Yuda. Miji hii ni mabomoko mpaka leo wala hakuna mutu anayeishi humo.


Kwa hiyo, kasirani yangu na hasira yangu iliwaka na kumwangika juu ya miji ya Yuda na barabara za Yerusalema, hata kukakuwa jangwa na mabomoko kama inavyokuwa mpaka leo.


Jinsi gani huo muji uliokuwa nyundo iliyoponda dunia nzima unavyoangushwa chini na kuvunjika! Babeli umekuwa pori tupu kati ya mataifa!


Nami nikauliza: Kuna mutu anayekuwa na hekima apate kueleza mambo haya? Ni nani aliyeongea na Yawe hata aweze kutangaza kwa nini inchi imeharibiwa na kufanywa tupu kama jangwa hata hakuna mutu anayepita humo?


Niliwaita wapenzi wangu, lakini wao wakanidanganya. Makuhani na wazee wangu wamekufia katika muji, wakijitafutia chakula kusudi wajirudishie nguvu zao.


Kwa hasira yake, Yawe amewaweka watu wa Sayuni katika giza. Ametupa toka mbinguni mpaka katika dunia utukufu wa Israeli. Kwa siku ya hasira yake, alilitupilia mbali hata hekalu lake.


Wazee wa Sayuni wameikaa chini kimya, wamejitia mavumbi juu ya vichwa na kuvaa gunia. Wabinti wa Yerusalema wameinamisha vichwa chini.


Namna gani zahabu yetu ilivyochakaa, zahabu safi kabisa ilivyobadilika! Mawe ya bei kali yamesambazwa kwa barabara zote.


Taji tuliojivunia imeanguka. Ole kwetu maana tumetenda zambi!


Wakubwa wote wa mataifa ya kandokando ya bahari watashuka toka kwenye viti vyao vya kifalme, na kuvua nguo zao za heshima pamoja na nguo zao zilizopindwa. Kisha kujaa hofu, wataikaa chini; nao watatetemeka wakati wote na kushangaa sana juu ya hayo yaliyokupata.


Wewe mwanadamu! Watu wa muji wa Tiro wameuchekelea Yerusalema na kusema: Aha! Yerusalema muji ambao watu wote walipitia, umeangamizwa! Sasa umetuachia nafasi; utajiri wake umeharibika!


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ndivyo itakavyokuwa juu ya Yerusalema. Mimi niliuweka kuwa katikati ya mataifa, umezungukwa na inchi za kigeni pande zote.


Miji yenu nitaiteketeza, pahali penu patakatifu nitapafanya jangwa na harufu zenu nzuri za sadaka sitazikubali.


Nitawatawanya ninyi kati ya watu wa mataifa na kuchomoa upanga juu yenu. Inchi yenu itakuwa ni ukiwa na miji yenu uharibifu.


Basi huu ndio muji uliojivuna na kuishi kwa usalama, muji uliojisemesha: Ni mimi tu, hakuna mwingine! Jinsi gani umekuwa mutupu na makao ya nyama wa pori! Kila mutu anayepita karibu atauzomea na kuuzarau.


Na kwa kadiri ulivyojitukuza na kuishi katika raha, kwa kadiri ile ile muuletee mateso na huzuni. Muji ule unajisemesha: ‘Mimi ninaikaa juu ya kiti cha kifalme kama vile malkia; mimi si mujane, wala sitapata huzuni hata kidogo!’


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ