Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Malaki 3:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Yawe wa majeshi alisema hivi: Mimi Yawe sibadiliki. Ni kwa sababu hii, ee ninyi wazao wa Yakobo, hamujateketezwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Malaki 3:6
36 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Siku hiyo, Yawe akafanya agano na Abramu akisema: “Ninawapa wazao wako inchi hii, toka muto Nili wa Misri mpaka ule muto mukubwa wa Furati,


Yawe akamwambia Abramu: “Mimi ni Yawe niliyekuleta toka Uri, muji wa Wakaldea, kusudi nikupe inchi hii uirizi.”


akamwambia: “Yawe anasema hivi: Nimeapa kwa nafsi yangu mwenyewe kwamba kwa sababu umefanya hivi, wala haukuninyima mwana wako wa pekee,


Wewe uliumba dunia tokea zamani, mbingu ni kazi ya mikono yako.


Vitatoweka na kuchakaa kama nguo, lakini wewe utabaki. Utavibadilisha kama nguo, navyo vitapita.


Lakini wewe unabaki sawasawa, na maisha yako hayana mwisho.


Lakini wema wa Yawe unadumu milele, kwa wale wote wanaomwabudu; na haki yake inadumu vizazi vyote,


Lakini Mungu mwenye huruma alisamehe uovu wao, wala hakuwaangamiza. Mara nyingi alizuia hasira yake, wala hakuacha kasirani yake yote iwake.


Lakini waligeuka na kufanya mabaya kama babu zao; wakayumbayumba kama upinde usiokuwa imara.


Mimi ndiye Yawe, Mungu wako, ndiye ninayeshika mukono wako. Mimi ndiye ninayekuambia: Usiogope, nitakusaidia.


Yawe, Mufalme na Mukombozi wa Israeli, Yawe wa majeshi anasema hivi: Mimi ni wa kwanza na wa mwisho; hakuna mungu mwingine isipokuwa mimi.


Mimi nitabaki yuleyule hata katika uzee wenu; hata katika wakati wenu wa imvi mimi nitawabeba. Nilifanya hivyo kwanza, nitafanya hivyo tena. Nitawabeba ninyi na kuwaokoa.


Mimi ni Yawe, Mungu wa watu wote. Hakuna lolote linaloweza kunishinda.


Halafu mufalme Dario akawaandikia watu wa makabila yote, mataifa yote, na luga zote katika dunia: Ninawatakia amani kwa wingi.


Nitaizuia hasira yangu kali; sitamwangamiza tena Efuraimu, maana mimi ni Mungu, wala si mwanadamu. Mimi ndimi Mutakatifu kati yenu, nami sitakuja kuwaangamiza.


Wewe si ndiwe Yawe, tangu zamani sana? Wewe ndiwe Mungu wangu, Mutakatifu wangu, usiyekufa. Ee Yawe, umewachagua Wakaldea watuhukumu! Ewe kimbilio letu, umewaimarisha kusudi watuazibu!


Mungu si mutu, hata aseme uongo, wala si mwanadamu, hata abadilishe nia yake! Ataahidi kitu na asikifanye, au kusema kitu asikitimize?


Basi ikiwa kama tulipokuwa waadui za Mungu tulipatanishwa naye kwa njia ya kufa kwa Mwana wake, inaonyesha zaidi sana kwamba tukiwa tumepatanishwa naye, tutaokolewa kwa njia ya uzima wa Kristo.


Ninajua hakika kwamba Mungu aliyeanza kazi hii njema ndani yenu, ataitimiza mpaka siku ile ya kurudi kwa Yesu Kristo.


Yesu Kristo ni yule yule, jana, leo na hata milele.


Basi kuna mambo mawili, ahadi na kiapo, yasiyoweza kubadilika, na kuelekea hayo, Mungu hawezi kusema uongo. Kwa hivi, sisi tuliomukimbilia tunatiwa moyo sana na kushika kwa nguvu tumaini tulilowekewa.


Kila zawadi nzuri na kila zawadi kamilifu inatoka juu kwa Mungu Baba aliyeumba miangaza yote inayokuwa katika mbingu. Mungu hawezi kubadilika wala kugeuka.


Bwana Mungu Mwenye Uwezo anasema: “Mimi ni Alfa na Omega.” Ni yeye anayekuwa, aliyekuwa na anayekuja.


Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho.”


Na Mungu ambaye ni utukufu wa Israeli hadanganyi, wala habadilishi wazo lake. Yeye si mwanadamu hata apate kubadilisha mawazo.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ