Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Malaki 3:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Lakini ni nani atakayevumilia siku ile atakapokuja? Ni nani atakayesimama kuvumilia atakapotokea? Yeye ni kama moto mukali unaosafisha chuma; ni kama sabuni ya mwenye kufua nguo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Malaki 3:2
47 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Akiwa pale, akatazama chini pande za Sodoma na Gomora na eneo lote la bonde, akashangaa kuona moshi ukipanda, moshi kama wa furu kubwa.


Hakika kuna nafasi ya kuchimba feza, na pahali ambako zahabu inasafishwa.


Ee Yawe, kama ungekumbuka maovu yetu, nani, ee Bwana wetu, angeweza kuishi?


Mufalme anasema: “Nitatangaza amri ya Yawe. Mungu aliniambia: ‘Wewe ni mwana wangu, mimi leo nimekuwa baba yako.


Ulipowakaripia, ee Mungu wa Yakobo, farasi na wapanda-farasi walipooza.


Toa takataka katika feza, na mufuaji wa vyuma atakutengenezea chombo kizuri.


Yawe anasema hivi: Mukuje basi, tukate shauri. Zambi zenu zikionekana kuwa nyekundu, zitakuwa nyeupe kama teluji; zikionekana kuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama sufu.


Wenye zambi katika Sayuni wanaogopa, wasiomwamini Mungu wanatetemeka na kusema: Nani anayeweza kuvumilia moto huu mukali? Nani anayeweza kuvumilia ndimi za moto usiozimika?


Bwana atawatakasa wanawake wa Sayuni toka uchafu wao na kusafisha damu iliyomwangika katika Yerusalema, kwa njia ya upepo wa hukumu na wa kuunguza.


Hata ukijisafisha kwa dawa ya kutosha taka na kutumia sabuni nyingi, madoa ya uovu wako yatabaki mbele yangu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Utaweza kuvumilia kuwa hodari siku nitakapokushambulia? Ni mimi Yawe ninayesema hivyo na nitakayetimiza hayo.


Wamoja kati ya wenye hekima watauawa, kusudi wapate kuondolewa uchafu, kutakaswa na kusafishwa, mpaka wakati wa mwisho, ambao sasa bado haujatimia.


Yawe anaamuru kundi lake kwa sauti; waaskari wake ni wengi sana, wanaomutii hawahesabiki. Siku ya Yawe kweli ni kubwa na ya kutisha sana! Nani atakayeweza kuivumilia?


Nani anayeweza kusimama mbele ya kasirani ya Yawe? Nani anayeweza kuvumilia ukali wa hasira yake? Yeye anaimwanga hasira yake inayowaka kama moto, hata mawe makubwa anayapasua vipandevipande.


Sehemu hiyo moja ya tatu itakayobaki, nitaipima na kuitakasa, kama vile mutu anavyosafisha feza, kama vile wanavyopima zahabu. Halafu wao wataniomba mimi, nami nitawajibu. Nitasema: Hawa ni watu wangu, nao watasema: Yawe, ndiye Mungu wetu.


Wale wajinga walipokwenda kununua mafuta, bwana-arusi akafika. Wale wenzao watano waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye katika karamu ya ndoa. Kisha mulango ukafungwa.


Nguo zake zikageuka nyeupe sana na kumetameta, wala katika dunia hakuna fundi wa kufua anayeweza kuziangarisha kama vile.


Simeoni akawabariki na kumwambia Maria, mama yake: “Mutoto huyu amezaliwa kwa sababu ya kuwaangusha na kuwasimamisha watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa kitambulisho kutoka kwa Mungu watu watakachokipinga,


Basi mukeshe na kuomba kila wakati, kusudi mupate nguvu ya kuepuka mambo hayo yote yatakayotokea, nanyi mupate kuweza kusimama mbele ya Mwana wa Mutu.”


Anashika lungo katika mikono yake kwa kupepeta ngano. Atakusanya ngano na kuitia katika gala yake, lakini atateketeza maganda katika moto usiozimika.”


Hata sasa shoka limekwisha kuwekwa tayari kwenye mashina ya miti. Kila muti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa katika moto.”


Heri mutu yule ambaye sitakuwa kikwazo kwake.”


Ninyi hamumujui, lakini mimi ninamujua. Kama ningesema kwamba simujui, ningekuwa mwongo kama ninyi. Lakini ninamujua na ninashika neno lake.


Basi muangalie vizuri kusudi musikatae kumusikiliza yule anayesema nanyi. Wale waliokataa kusikiliza yule aliyewaonya hapa katika dunia hawakuponyoka azabu ya Mungu. Si jambo hilo linaonyesha wazi kwamba sisi hatutaweza kuponyoka kama tunamugeuzia mugongo yule anayetutolea maonyo kutoka mbinguni?


Yule bibi amepewa nguo ya kuvaa iliyofumwa na nyuzi nzuri zenye kungaa. (Nguo ile ni mufano wa matendo ya haki ya watu wa Mungu.)


Nitawaua wafuasi wake. Na hivi makanisa yote yatajua kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo ya watu na mafikiri yao. Vilevile yatajua kwamba mimi nitamulipa kila mumoja wenu kufuatana na matendo yake.


Kwa maana siku kubwa ya kasirani yao imekuja. Ni nani atakayeweza kusimama imara?”


Nami nikamujibu: “Bwana wangu wewe ndiwe unayejua.” Naye akaniambia: “Hawa ndio wanaotoka katika mateso makubwa. Wamesafisha kanzu zao na kuzifanya kuwa nyeupe katika damu ya Mwana-Kondoo.


Kisha, wakaaji wa muji wa Beti-Semesi wakasema: “Nani anayeweza kusimama mbele ya Yawe, huyu Mungu mutakatifu? Atakwenda kwa nani kusudi aondoke kwetu?”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ