Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Malaki 3:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Halafu watu wanaomutii Yawe walizungumuza wao kwa wao, naye Yawe akasikia mazungumuzo yao. Mbele yake kukawekwa kitabu ambamo uliandikwa ukumbusho wa wale wanaomutii na kumuheshimu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Malaki 3:16
64 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Malaika akamwambia: “Usinyooshe mukono wako juu ya kijana wala usimufanyie jambo lolote! Sasa ninajua kwamba unamwogopa Mungu, maana haukuninyima hata mwana wako wa pekee.”


Wakati mufalme Daudi alipokuwa akikaa katika nyumba yake ya kifalme, naye Yawe amemwezesha kuwa na amani na waadui zake kila upande,


Ninaogopa kwamba mara tu nitakapoondoka, Roho wa Yawe atakunyanyua na kukupeleka pahali nisipopajua! Nikienda kumwambia Ahabu kwamba uko hapa, naye akikutafuta na asikupate, ataniua mimi, ingawa mimi mutumishi wako ninamwogopa Yawe tangu ujana wangu.


Basi, Ahabu akamwita Obadia musimamizi wa nyumba ya kifalme. Obadia alikuwa mutu anayemwogopa Yawe sana,


“Kwa hiyo, baba yangu Daudi alikusudia kujenga nyumba ambamo Yawe, Mungu wa Israeli, atakamoabudiwa.


Ee Bwana, usikilize maombi yangu mimi mutumishi wako na ya watumishi wako wanaofurahia kukutii wewe. Ninakuomba unifanikishe leo, mimi mutumishi wako, na kunijalia kuhurumiwa na mufalme.” Mimi nilikuwa na madaraka ya kumupa mufalme kinywaji.


Uchunguzi ulipofanywa, iligunduliwa kwamba ni kweli; basi, watu hao wawili wakatundikwa juu ya muti. Habari juu ya tukio hilo iliandikwa katika kitabu cha Mambo ya Siku mbele ya mufalme.


Usiku ule, mufalme hakupata usingizi. Basi, akaamuru kitabu cha Mambo ya Siku cha matukio ya kila siku, kiletwe, nacho kikasomwa mbele yake.


Kisha Mungu akamwambia mwanadamu: Sikia! Kumwogopa Bwana ndiyo hekima, na kujitenga na uovu ndiyo maarifa.


Katika majivuno yake anasema: “Mungu hatagundua. Hakuna Mungu.” Hayo ndiyo mawazo yake yote.


Nitamwimbia Yawe maisha yangu yote; nitamusifu Mungu wangu muda wote nitakaoishi.


Kumwogopa Yawe ni musingi wa hekima; wote wanaotii amri zake wanajaliwa akili. Sifa zake zinadumu milele.


atawabariki wote wanaomwabudu, atawabariki wakubwa kama vile wadogo.


Mimi ni rafiki ya wote wanaokuheshimu, rafiki ya wanaoshika kanuni zako.


Mbele sijasema neno lolote, wewe, ee Yawe, unalijua kabisa.


lakini anapendezwa na watu wanaomuheshimu, ndio wanaotegemea wema wake.


Na juu ya waaminifu katika inchi, ninaheshimu nguvu zao.


Ninajua Yawe atamusaidia mufalme aliyemuchagua, atamujibu tokea pahali pake patakatifu mbinguni; kwa mukono wake wenye nguvu atamujalia ushindi mukubwa.


Yawe anawaangalia wale wanaomwabudu, watu ambao wanatumainia wema wake.


Ujiepushe na uovu, utende mazuri; utafute amani na kuifuatilia.


Ee Mungu, uwalipe kwa kadiri ya uovu wao, uwaangushe hao waovu kwa hasira yako.


Wewe unajua kutangatanga kwangu; unaweka machozi yangu ndani ya chupa. Yote yanakuwa katika kitabu chako.


Enyi munaomwabudu Mungu, mukuje wote musikilize, nami nitawaelezea mambo aliyonitendea.


Mahangaiko ya moyo wangu yanapozidi, wewe unanifariji na kunifurahisha.


Lakini sasa, ninakuomba uwasamehe zambi yao. Ikiwa hautawasamehe, ninakusihi unifute mimi katika kitabu chako ambamo uliwaandika watu wako.


Anayeandamana na wenye hekima anapata hekima, lakini anayejiunga na wapumbafu atapata hasara.


Ee Mungu, unawaweka katika amani wanaokuwa imara, unawaweka katika amani kwa sababu wanakutegemea.


Katika njia ya maamuzi yako tunakungojea ee Yawe; tamaa yetu ni kulikumbuka jina lako.


Wale watakaobaki wazima katika Yerusalema, huko Sayuni, wataitwa Wachaguliwa wa Mungu; hao ndio wale wote watakaokuwa wameandikwa katika kitabu chake waishi huko Yerusalema.


Nani kati yenu anayemwogopa Yawe? Nani anayetii maneno ya mutumishi wake? Kama kuna mutu anayetembea katika giza bila taa, amutumainie Yawe, na kumutegemea Mungu wake.


Mujue kwamba mambo hayo yameandikwa mbele yangu, sitanyamaza lakini nitawalipiza; nitawalipa sawa inavyostahili.


Nimesikia Efuraimu akilalamika hivi: Umeniazibu vikali, maana nilikuwa kama mwana-ngombe asiyezoea nira. Unigeuze nami nitakugeukia, maana wewe ndiwe Yawe, Mungu wangu.


Mimi nilisikiliza kwa uangalifu, lakini wao hawakusema ukweli wowote. Hakuna mutu anayetubu uovu wake, wala kujiuliza hivi: Nimefanya nini? Kila mumoja wao anashika njia yake, kama farasi anavyokimbia haraka kwa vita.


akamwambia hivi: Pita katikati ya Yerusalema, upate kutia kitambulisho kwenye vipaji vya nyuso za watu wanaohuzunika na kulia kwa sababu ya machukizo yote yanayotendeka katika muji huu.


Wakati huo, Mikaeli, malaika mukubwa, anayekuwa mulinzi wa watu wako, atatokea. Halafu kutakuwa wakati wa taabu sana kuliko nyakati zingine zote tangu mataifa yalipoanza kuwa katika dunia. Lakini, wakati huo, kila mumoja wa watu wako ambaye jina lake limeandikwa katika kitabu cha uzima, ataokolewa.


Kutoka kiti hicho kijito cha moto kilibubujika, kikatiririka. Maelfu ya watu walimutumikia, na mamilioni walisimama mbele yake. Halafu waamuzi wakajitayarisha kwa kuhukumu, na vitabu vikafunguliwa.


Yawe wa majeshi anasema: Kisha nitawakaribia kwa kuwahukumu. Sitasita kutoa ushuhuda juu ya wachawi, wazinzi, watoa ushuhuda wa uongo, wanaopunja mushahara wa watumishi, wanaowatesa wajane na wayatima, wanaozuia mugeni asipate haki yake na wale wasioniogopa mimi.


Basi, akafika saa ile ile, akaanza kumushukuru Mungu. Naye akaeleza habari za mutoto huyo kwa watu wote waliokuwa wakingojea jinsi Mungu atakavyokomboa Yerusalema.


Walipofika katika muji wakapanda katika chumba cha gorofi walipokuwa wanazoea kukutanana. Na waliokuwa pale ni hawa: Petro, Yoane, Yakobo, Andrea, Filipo, Toma, Bartolomayo, Matayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni wa kikundi cha Wazeloti na Yuda mwana wa Yakobo.


Yeye alikuwa mwenye kuogopa Mungu, naye alimwabudu Mungu pamoja na watu wote waliokuwa kwake. Aliwasaidia wamasikini wengi, naye alikuwa akimwomba Mungu siku zote.


Wakati siku ya Pentekoste ilipotimia, wanafunzi walikuwa wamekusanyika wote pamoja wakibaki kwenye nafasi moja.


Wakati ule, kanisa lilikuwa na amani katika Yudea yote, Galilaya na Samaria. Vilevile lilizidi kupata nguvu na kuendelea kumwogopa Bwana, nalo liliongezeka kwa musaada wa Roho Mutakatifu.


Munapoongea, museme maneno ya zaburi, mumusifu Bwana na kumwabudu kwa nyimbo za kiroho. Mumwimbie na kumushangilia kwa moyo wenu wote.


Basi mufarijiane na kujengana imani, kama vile munavyozoea kufanya.


Tunawasihi wandugu, muwaonye wale wanaokuwa wavivu, muwatie moyo wale wanaoregea, muwasaidie wale wanaokuwa zaifu, na mukuwe wavumilivu kwa watu wote.


Tena tushugulikiane kusudi tupate kuvutana sisi kwa sisi kuwa na upendo na kufanya mema.


Muangalie vizuri, kusudi hata mutu mumoja asijikoseshe mwenyewe kupata neema ya Mungu, wala asikuwe sawa shina la mumea unaotoa matunda machungu na kuleta fujo kati yenu na kuambukiza watu wengi.


Lakini muonyane kila siku kwa muda wote ambao lile neno “leo” linalotajwa lingali linatuelekea kusudi hata mumoja wenu asikuwe mugumu kwa kudanganywa na zambi.


Ewe Bwana, hakuna asiyekuogopa, wala hakuna asiyekutukuza, kwa maana wewe peke yako ndiwe mutakatifu. Mataifa yote yatakuja kukuabudu, kwa maana matendo yako ya haki yameonyeshwa wazi.”


Nikaona wale waliokufa, wakubwa na wadogo wakisimama mbele ya kile kiti cha kifalme. Vitabu vikafunguliwa na kitabu kingine kikafunguliwa ndicho kitabu cha uzima. Wale waliokufa wakahukumiwa kufuatana na matendo yao sawa vile ilivyoandikwa katika vitabu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ