Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Malaki 3:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Tunayoona sisi, ni kwamba wenye kiburi ndio wenye furaha siku zote. Watu waovu, ingawa wanastawi, hata wanapomujaribu Mungu, hawapati azabu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Malaki 3:15
37 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata hivyo, akajizuia, akaenda kwake. Halafu akawaalika kwake warafiki zake, na kumwomba muke wake Zeresi ajiunge nao.


Katika mambo haya yote Yobu hakutenda zambi wala hakumushitaki Mungu kuwa na kosa.


Makao ya wanyanganyi yana amani. Wenye kumuchokoza Mungu wako salama; nguvu yao ni mungu wao.


Mwovu anaponyeshwa siku ya hasara, anaokolewa siku ya kasirani!


Ukimurudilia Mungu na kunyenyekea, ukiondoa uovu mbali na makao yako,


Mwovu anajisifia tamaa zake mbaya, anapata faida kwa njia mbaya, anazarau na kumukataa Yawe.


Walipatwa na tamaa kubwa kule katika jangwa, wakamupima Mungu kule kwenye ukiwa.


Unikinge nisielekee kufanya mabaya, nisijishugulishe na matendo maovu, nisijiunge na watu wanaotenda mabaya, wala nisishiriki hata kidogo katika karamu zao.


Maana atakapokufa hatachukua kitu chochote, mali yake haitashuka huko chini pamoja naye.


Enyi watawala, munasema kwa haki kweli? Munawahukumu watu kwa usawa?


Hivi ndivyo watu waovu wanavyokuwa; wako na kila kitu, nao wanapata hata zaidi.


maana niliwaonea wivu wenye kiburi, nilipoona wakosaji wakifanikiwa.


Walimujaribu Mungu kwa makusudi; wakidai wapewe chakula walichotaka.


Walimujaribu Mungu tena na tena, wakamukasirikisha huyo Mutakatifu wa Israeli.


Hata hivyo walimupima na kumwasi Mungu Mukubwa; wala hawakushika maagizo yake.


babu zenu waliponijaribu na kunipima, ingawa walikuwa wameona mambo niliyowatendea.


Matumaini ya waovu yanaporomoka na kuharibika, lakini mutu mwenye haki anasimama imara.


Kuna jambo moja la bure nililotambua hapa katika dunia: mara kwa mara watu wema wanatendewa jinsi waovu wanavyostahili kutendewa, nao waovu wanatendewa jinsi watu wema wanavyostahili kutendewa. Ninasema kwamba hayo nayo ni bure.


Usimutumainie mwanadamu, uzima wake ni kama pumzi tu. Yeye anafaa kitu gani?


Kisha, mutakuja na kusimama mbele yangu katika hekalu hili linalojulikana kwa jina langu na kusema “Tuko salama”, ingawa munaendelea kufanya mambo hayo yanayonichukiza.


Mara moja jambo hilo juu ya mufalme Nebukadneza likatimizwa. Alifukuzwa mbali na wanadamu, akakuwa anakula majani kama ngombe. Alilowanishwa na umande wa mbinguni, na nywele zake zikakuwa ndefu kama manyoya ya tai, na kucha zake kama za ndege.


Wale watu kwa pamoja wakamwendea mufalme Dario na kumwambia: Ee mufalme, ujue kwamba hakuna sheria wala amri yoyote ya Wamedi na Wapersi inayoweza kubadilishwa kisha kuwekwa na mufalme.


Mumemuchokesha Yawe kwa maneno yenu matupu. Hata hivyo, munasema: Tumemuchokesha namna gani? Mumemuchokesha munaposema: Yawe anawaona kuwa wazuri watu wanaotenda mabaya; tena anawapenda. Au munapouliza: Yuko wapi yule Mungu mwenye haki?


Halafu kwa siku ile iliyopangwa, Herode akavaa nguo zake za kifalme, akaikaa katika kiti chake cha kifalme na kuwatolea watu hotuba.


Halafu Petro akamwambia: “Namna gani mulipatana kwa kumupima Roho wa Bwana? Sikiliza! Wale wanaotoka kumuzika mume wako wamefika hapa kwenye mulango, nao watakupeleka vilevile.”


Vilevile tusimupime Bwana kama vile wamoja wao walivyofanya, hata wakauawa na nyoka.


Kule babu zenu walinipima na kunijaribia, ingawa walikuwa wameona yote niliyotenda kwa muda wa miaka makumi ine.


Na hivi vilevile, ninyi vijana, munapaswa kuwatii hao wazee. Ninyi wote munapaswa kuwa na unyenyekevu, mupate kutumikiana; maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mungu anawapinga wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ