Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Malaki 3:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Mulete katika gala yangu zaka yote, kusudi katika nyumba yangu kuwe chakula cha kutosha. Kisha munaweza kunijaribu. Munipime namna hiyo nanyi mutaona kama sitayafungua madirisha ya mbinguni na kuwatiririshia baraka tele.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Malaki 3:10
35 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nalo jiwe hili nililosimika hapa kama nguzo, litakuwa nyumba yako Mungu, nami nitakupa sehemu ya kumi ya vitu vyote utakavyonipa.”


Noa alipokuwa na umri wa miaka mia sita, katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa pili, siku hiyo chemichemi zote za vilindi vya udongo zikabubujika maji, na madirisha ya mbinguni yakafunguka.


Yule jemedari mulinzi wa mufalme alikuwa amemwambia Elisha: “Hata kama Yawe mwenyewe angefanya madirisha mbinguni, jambo hilo litawezekana?” Naye Elisha alikuwa amemujibu: “Utaona kwa macho yako mwenyewe, lakini wewe hautakula.”


Jemedari mulinzi wa mufalme akamwambia Elisha: “Hata kama Yawe mwenyewe angefanya madirisha mbinguni, jambo hilo litawezekana?” Elisha akamujibu: “Utaona kwa macho yako mwenyewe, lakini wewe hautakula.”


Kati ya Walawi, Ahia alielekea uangalizi wa hazina ya nyumba ya Mungu, na hazina na vitu vitakatifu.


Wakati ule wakachagua watu wa kuchunga vyumba vya gala ambamo matoleo kwa ajili ya hekalu yaliwekwa, malimbuko ya kwanza, zaka na kuyakusanya kutoka katika mashamba ya miji, kwa ajili ya makuhani na Walawi kama ilivyotakiwa na Sheria. Watu wote wakafurahia makuhani na Walawi waliotumika,


Watu wote wa Israeli, tangu wakati wa Zerubabeli na Nehemia, walitoa matoleo ya kila siku kwa ajili ya waimbaji na walinzi wa milango. Zaidi ya yote, watu wa Israeli wakatoa matoleo kwa ajili ya Walawi, nao Walawi wakatenga sehemu kwa ajili ya wazao wa Haruni.


alimuruhusu Tobia kutumia chumba kikubwa ambamo pale mbele walikuwa wakiweka sadaka za unga, ubani, vyombo, zaka za unga, divai, mafuta; vitu hivyo vyote Waisraeli walivyoagizwa kutoa kwa Walawi, waimbaji, walinzi wa milango, na matoleo kwa makuhani.


Umutumainie Yawe na kutenda mazuri, upate kuishi katika inchi na kuwa salama.


Hata hivyo aliamuru mawingu, akafungua milango ya mbingu;


Mawingu yakijaa maji, mvua inanyesha. Muti ukiangukia upande wa kusini au wa kaskazini, pale unapoangukia ndipo unapolala.


Nitawafanya waishi kandokando ya mulima wangu mutakatifu na kuwabariki. Nitawaletea mvua kwa wakati wake, nazo zitakuwa mvua za baraka.


Sehemu ya kwanza ya malimbuko yenu na vya matoleo yenu ya kila aina vitakuwa kwa ajili ya makuhani. Tena mutawapa sehemu ya kwanza ya unga wenu, kusudi mulete baraka juu ya nyumba zenu.


Nitakufanya muke wangu milele; ukuwe wangu kwa sheria na haki, kwa wema na huruma.


Alisikiliza, akajibu maombi yao, akasema: Sasa nitawapa tena ngano, divai na mafuta, nanyi mutashiba navyo. Sitawafanya muzarauliwe tena na mataifa.


Nafasi ya kupepetea itajaa ngano, vikamulio vitafurika divai na mafuta.


Wakati wa mavuno mutakuwa mungali munakula mazao ya zamani. Tena itawapasa kuondoa yaliyobaki kwa kupata nafasi ya kulinda mavuno mapya.


Kama mukifuata masharti yangu na kushika amri zangu,


Zaka za mazao ikuwe ni ngano au matunda ya miti, yote ni mali ya Yawe. Yote ni takatifu kwa Yawe.


Ingawa sasa hakuna ngano ndani ya gala, nayo mizabibu, tini, mikomamanga na mizeituni haijazaa kitu, lakini tangu leo, nitawabariki.


Kuelekea Walawi, hao nimewapa sehemu ya kumi ya kila kitu Waisraeli wanachonitolea kuwa urizi wao. Haya yatakuwa malipo yao kwa kazi wanayotoa katika kulitunza hema la mukutano.


Lakini ninyi mushugulikie kwanza Ufalme wa Mungu na kufuata haki mbele yake, naye atawaongezea vitu vile vyote.


Vilevile huko mutapeleka sadaka zenu za kuteketezwa kwa moto na sadaka zingine, sehemu ya kumi za mazao yenu, matoleo yenu ya mapenzi na ya kutimiza kiapo, na wazaliwa wa kwanza wa ngombe na kondoo wenu.


“Mutoe sehemu ya kumi ya mazao yenu yote ya shamba kila mwaka.


Hiyo itakuwa kwa ajili ya Walawi, kwa sababu hawana fungu wala urizi wao kati yenu, nao wageni, wayatima na wajane ambao wanaishi katika miji yenu, watakuja kula na kushiba. Mufanye hivi naye Yawe, Mungu wenu, atawabariki katika kazi zenu zote munazofanya kwa mikono yenu.


Yawe atawafungulia hazina yake nzuri kutoka mbinguni na kunyesha mvua katika inchi kwa wakati wake, na kubariki kazi zenu. Mutakopesha mataifa mengi, lakini ninyi hamutakopa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ