Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Malaki 3:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Yawe wa majeshi anasema: Ninamutuma mujumbe wangu anitangulie kunitengenezea njia. Bwana munayemutafuta atalifikia hekalu lake kwa rafla. Mujumbe munayemutazamia kwa hamu kubwa atakuja na kutangaza agano langu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Malaki 3:1
38 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Zaburi ya Daudi. Yawe anamwambia bwana wangu: “Ikaa na mamlaka kwa kuume kwangu mpaka nitakapowaweka waadui zako chini ya miguu yako.”


Muangalie, mimi ninamutuma malaika awatangulie katika safari kusudi awalinde na kuwafikisha katika inchi niliyowatayarishia.


Musikilize na kutii maneno atakayosema, wala musimwasi. Hatawasamehe uasi wenu maana nimemutuma kwa jina langu.


Bwana wetu Yawe anakuja na nguvu, kwa mukono wake anatawala. Yeye anakuja na mapato yake, anafika na mushahara wake.


Katika taabu zao zote, hakumutuma mujumbe mwingine kwa kuwasaidia, lakini yeye mwenyewe alikuja kuwaokoa; kwa upendo na huruma yake aliwakomboa. Aliwabeba na kuwakamata tangu zamani.


Basi, Bwana mwenyewe atawapa kitambulisho: bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume na kumwita jina lake “Emanueli – Mungu Yuko Pamoja Nasi”.


Utawala wake utastawi siku zote, amani ya ufalme wake haitakoma. Atakamata madaraka ya mufalme Daudi na kutawala juu ya ufalme wake; ataustawisha na kuuimarisha kwa kufuata sheria ya Mungu na kutenda kwa haki tangu sasa na hata milele. Yawe wa majeshi atafanya mambo hayo.


Kisha Hagai, mujumbe wa Yawe, akawapa watu ujumbe huu kutoka kwa Yawe: Mimi niko pamoja nanyi. –Ni ujumbe wa Yawe.


Hivyo mutajua kwamba nimewapa amri hii kusudi agano langu na ukoo wa Lawi likuwe la kudumu.


Ni kazi ya makuhani kuwafundisha watu maarifa ya kweli juu ya Mungu kusudi watu wawaendee kwa kujifunza mapenzi yangu kwao, maana makuhani ni wajumbe wa Yawe wa majeshi.


Na ikiwa munasadiki, Yoane ndiye nabii Elia aliyepaswa kuja.


Na wewe, mutoto wangu, utaitwa nabii wa Mungu Mukubwa, maana utatangulia mbele ya kufika kwa Bwana, kusudi umutengenezee njia.


Yesu alikuwa akifundisha kila siku ndani ya hekalu. Lakini wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria pamoja na wakubwa wa watu wakatafuta kumwua.


Leo hii Mwokozi amezaliwa kwa ajili yenu katika muji wa Daudi, yeye ndiye Kristo na Bwana.


Basi, akafika saa ile ile, akaanza kumushukuru Mungu. Naye akaeleza habari za mutoto huyo kwa watu wote waliokuwa wakingojea jinsi Mungu atakavyokomboa Yerusalema.


Nyuma ya siku tatu, wakamukuta ndani ya hekalu, akiikaa katikati ya walimu wakubwa wa Sheria, akiwasikiliza na kuwauliza maulizo.


Paulo akawaambia: “Yoane aliwabatiza wale waliogeuka toka zambi zao na kuwaambia Waisraeli kwamba wamwamini yule atakayekuja nyuma yake, naye ndiye Yesu.”


Na wakati ule kulipokuwa mukutano wa Waisraeli katika jangwa, yeye alikuwa pale pamoja na babu zetu na yule malaika aliyesema naye kwenye mulima Sinai. Na ni yeye aliyefunuliwa ujumbe wa Mungu unaoleta uzima na kuutangaza kwetu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ