Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Malaki 2:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Nami vilevile nitawafanya muzarauliwe na kuchekelewa na Waisraeli, kwa sababu hamukuzifuata njia zangu, na munapowafundisha watu wangu munapendelea wamoja kati yao. –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Malaki 2:9
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu Mikaya alisema: “Ukirudi salama basi, utajua kwamba Yawe hakusema nami.” Kisha akaendelea kusema: “Musikilize enyi watu wote!”


Sitamupendelea mutu yeyote wala kutumia maneno ya kubembeleza mutu,


Mwenye haki anakumbukwa kwa baraka, lakini waovu watasahauliwa kabisa.


Mutu anasifiwa kadiri ya hekima yake, lakini mwenye moyo wa mafikiri mabaya anazaruliwa.


Nitavirarua vitambaa vyenu na kuwaokoa watu wangu toka katika mikono yenu; nao hawatakuwa tena kama nyama wa kuwindwa katika mikono yenu. Halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe.


Watapata hasara kwa mufululizo; nazo habari mbaya zitafuatana. Watamwomba nabii awatabirie. Makuhani hawatakuwa na sheria yoyote; na wazee watakosa shauri la kuwapatia.


Waamuzi wanahukumu kwa kupewa kutuliro, makuhani wake wanafundisha kwa kupata malipo, manabii wanatabiri kwa kupata feza. Hata hivyo wanajidai kumutegemea Yawe, wakisema: Yawe, si yupo pamoja nasi? Hatutapatwa na hasara yoyote!


Nitakutupia uchafu, na kukuzaraulisha, na kukufanya kuwa mushangao kwa watu.


Nitawaazibu watoto wenu na ninyi wenyewe kutokana na uovu wenu, na kuzipakaa nyuso zenu mavi ya nyama wenu wa sadaka. Nitawafukuza mbali nami.


Lakini ninyi makuhani mumegeuka na kuacha njia ya haki. Mafundisho yenu yamewaongoza watu wengi katika kutenda mabaya. Mumelivunja agano nililofanya nanyi.


Lakini kwa kutaka kujipatia haki, yeye akamwuliza Yesu: “Mwenzangu ni nani?”


“Ole kwenu, ninyi Wafarisayo! Munatoa fungu moja la kumi la vijani vya kukoleza chakula na kila namna ya mboga; lakini mumezarau haki na upendo wa Mungu. Mambo hayo ndiyo mulipaswa kushika pasipo kuacha mengine.


Lakini kuelekea wale waliohesabiwa kuwa waongozi, hainifalii kitu kujua cheo gani walichokuwa nacho, kwa maana Mungu hahukumu kwa kuangalia mambo ya inje. Watu wale hawakunifundisha kitu kipya.


Musipendelee mutu yeyote katika kutoa hukumu; mutawasikiliza bila upendeleo, wakubwa kwa wadogo. Musiogopeshwe na sura ya mutu, maana ninyi mutapaswa kuhukumu kwa ajili ya Mungu. Kukikuwa maneno ambayo ni magumu sana kwenu, mutayafikisha kwangu nami nitayasikiliza.’


Kwa hiyo, ujumbe wa Yawe, Mungu wa Israeli, ni huu: Niliahidi kwamba jamaa yako na jamaa ya babu yako mutakuja mbele yangu kunitumikia milele; lakini sasa jambo hilo likuwe mbali nami. Nitawaheshimu wale wanaoniheshimu, na wale wanaonizarau, nitawazarau. –Ni ujumbe wa Yawe.–


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ