Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Malaki 2:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Lakini ninyi makuhani mumegeuka na kuacha njia ya haki. Mafundisho yenu yamewaongoza watu wengi katika kutenda mabaya. Mumelivunja agano nililofanya nanyi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Malaki 2:8
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Uria akajenga mazabahu ile kulingana na mufano ule na kuimaliza mbele ya kurudi kwa Ahazi.


Ee Mungu, kumbuka jinsi watu walivyochafua ukuhani na agano la kikuhani na la Walawi.


Sikugeuka mbali na maamuzi yako, maana wewe mwenyewe ulinifundisha.


Yawe alinitendea kwa kadiri ya haki yangu; alinilipa kwa vile mikono yangu haina kosa.


Mutu anasifiwa kadiri ya hekima yake, lakini mwenye moyo wa mafikiri mabaya anazaruliwa.


Mugeuke na kuiacha njia ya ukweli; musituambie tena juu ya Mungu, Mutakatifu wa Israeli.


Tumekuasi na kukukana, ee Yawe, tumekataa kukufuata, ewe Mungu wetu. Tunasema maneno ya kutesa na uasi, katika mioyo yetu tunatunga na kutoa maneno ya uongo.


Kwa hiyo, Yawe hawahurumii vijana wao, hana huruma juu ya wayatima na wajane wao; maana hakuna hata mumoja anayemufuata, kila mutu anasema upumbafu. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


Ee Yawe, tumaini la Waisraeli, wote wanaokukataa wafezeheshwe. Wanaokuacha wewe watatoweka, kama majina yaliyoandikwa chini katika mavumbi, kwa maana wamekuacha wewe Yawe, unayekuwa chemichemi ya maji ya uzima.


Yawe anasema hivi: Alaaniwe mutu anayemutegemea mwanadamu, mutu ambaye anategemea nguvu za mwanadamu, mutu ambaye moyo wake umegeuka mbali nami Yawe.


Lakini watu wangu wamenisahau mimi, wanaifukizia miungu ya uongo ubani. Wamejikwaa katika njia zao, wameacha barabara zao za zamani.


Nao makuhani hawakujiuliza hivi: Yuko wapi Yawe? Wafundi wa sheria hawakunijua, viongozi wa watu waliniasi; manabii nao walitabiri kwa jina la Bali na kuabudu sanamu zisizokuwa na faida yoyote.


Makuhani wao wanavunja sheria zangu, na kukufuru vyombo vyangu vitakatifu. Hawapambanui kati ya vitu vitakatifu na vitu visivyokuwa vitakatifu, wala hawafundishi watu tofauti kati ya mambo yanayokuwa machafu na yanayokuwa safi. Wameacha kuzishika Sabato zangu, na kunizaraulisha kati yao.


Walawi walioniacha wakati ule Waisraeli walipojitenga nami kwa kufuata miungu yao, watabeba azabu yao.


Lakini kwa sababu waliongoza ibada za miungu kwa ajili ya watu wa Israeli, wakasukuma watu kutenda zambi, basi, nimeunyoosha mukono wangu kuwaazibu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Nao watabeba azabu yao.


Mumelichafua hekalu langu kwa kuruhusu waingie humo watu wasiotahiriwa, watu wasionitii mimi, wakati mafuta na damu vinatolewa kwa ajili yangu. Hivyo, ninyi watu wangu mumelivunja agano langu kwa machukizo yenu yote.


Watu wangu wameangamia kwa kutonijua, maana wewe kuhani umekataa mafundisho. Nimekukataa kuwa kuhani wangu. Kwa maana umeisahau sheria ya Mungu wako, nami vilevile nitawasahau watoto wako.


kusudi asichafue watoto wake mwenyewe. Mimi ni Yawe niliyemutakasa.


Manabii wake ni watu wasiojali na wadanganyifu. Makuhani wake wamevichafua vitu vitakatifu na kuivunja sheria kwa nguvu.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Mutoto anamuheshimu muzazi wake, na mutumishi anamuheshimu bwana wake. Ikiwa mimi ndiye Baba wenu, mbona munanivunjia heshima? Ikiwa mimi ni bwana wenu, mbona hamuniheshimu? Ninasema hivyo kwa ninyi makuhani munaozarau jina langu. Nanyi munauliza: Sisi tumezarau jina lako namna gani?


Katika agano hilo, niliwaahidi uzima na amani na kwamba wao wanapaswa kunitii mimi, nao kwa upande wao walinitii mimi na kuogopa jina langu.


Kwa hiyo umwambie kwamba ninafanya naye agano la amani.


Ninaagana naye kwamba yeye na wazao wake watakuwa makuhani milele kwa sababu aliona wivu kwa ajili yangu mimi Mungu wake, akawafanyia Waisraeli upatanisho.


Ni vema kuacha kula nyama, kunywa divai na kujizuiza kufanya chochote kinachoweza kumukwaza ndugu yako.


Basi wandugu zangu, muangalie vizuri, kati yenu kusikuwe mutu mumoja mwenye moyo mubaya wa kutokuamini, aliyefikia hata kujitenga mbali na Mungu Mwenye Uzima.


Zambi hii ya vijana hao wa Eli ilikuwa kubwa sana mbele ya Yawe. Maana, vijana hao walizarau matoleo ya Yawe.


Musifanye hivyo wana wangu, kwa sababu mambo hayo ninayoyasikia kutoka kwa watu wa Yawe ni mabaya.


Kwa hiyo, ujumbe wa Yawe, Mungu wa Israeli, ni huu: Niliahidi kwamba jamaa yako na jamaa ya babu yako mutakuja mbele yangu kunitumikia milele; lakini sasa jambo hilo likuwe mbali nami. Nitawaheshimu wale wanaoniheshimu, na wale wanaonizarau, nitawazarau. –Ni ujumbe wa Yawe.–


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ