Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Malaki 2:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Mumemuchokesha Yawe kwa maneno yenu matupu. Hata hivyo, munasema: Tumemuchokesha namna gani? Mumemuchokesha munaposema: Yawe anawaona kuwa wazuri watu wanaotenda mabaya; tena anawapenda. Au munapouliza: Yuko wapi yule Mungu mwenye haki?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Malaki 2:17
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Anayetawala ulimwengu kwa sheria zake anachukia haki? Utasubutu kumuhukumu mwenye haki na mwenye nguvu,


Heri Yobu angechunguzwa mpaka mwisho, kwa maana anajibu kama watu waovu.


Lakini sasa umehukumiwa kama mwovu, hukumu ya haki imekupata.


Inchi ikitiwa katika utawala wa mwovu, Mungu anafunga macho ya waamuzi wake! Kama si yeye anayefanya hivyo, ni nani basi?


Kwa vile uovu hauazibiwi haraka, mioyo ya wanadamu inakusudia kutenda mabaya.


Sipendezwi na sikukuu zenu za mwandamo wa mwezi, pamoja na sikukuu zenu zingine. Zimekuwa muzigo muzito kwangu, nami nimechoka kuzivumilia.


Ole kwenu ninyi munaomuficha Yawe mipango yenu, munaotenda matendo yenu katika giza na kusema: Hakuna atakayetuona; nani anayeweza kujua tunachofanya?


Hata hivyo, Yawe anangoja kuwasamehe, atasimama na kuwaonea huruma. Yawe ni Mungu wa haki. Heri wote wale wanaomutumainia.


Lakini ewe taifa la Yakobo, haukuniabudu mimi; enyi watu wa Israeli, mulichoka nami!


Hamukuninunulia marasi kwa mali yenu, wala kunishibisha kwa mafuta za sadaka. Pahali pake zambi zenu zimekuwa muzigo kwangu, mumenichokesha kabisa kwa makosa yenu.


Basi, Isaya akamujibu: Musikilize basi, enyi watu wa ukoo wa Daudi! Haitoshi kuwachokesha watu hata sasa munataka kumuchokesha Mungu wangu vilevile?


Ee Yawe, wewe ni mwenye haki, ingawa nitakushitaki. Lakini ningependa nibishane nawe juu ya mambo ya haki: Kwa nini waovu wanafanikiwa katika mambo yao? Mbona wote wanaodanganya wanastawi?


Ninyi mumenikataa mimi. –Ni ujumbe wa Yawe.– Ninyi mumeniacha na kurudi nyuma. Kwa hiyo nimenyoosha mukono kwa kuwaangamiza. Nimechoka na kuwahurumia.


Angalia jinsi watu wanavyoniambia: Vile vitisho vya Yawe viko wapi? Vifike basi!


Yawe hakuweza kuvumilia tena matendo yenu maovu na mambo ya kuchukiza muliyotenda; ndiyo maana inchi yenu imekuwa ukiwa, jangwa, laana na bila wakaaji, kama inavyokuwa mpaka leo.


Wewe umesahau yale ambayo mimi nilikufanyia ulipokuwa kijana. Wewe umenichukiza sana kwa mambo yale yote. Basi, nitakulipiza kisasi juu ya kila kitu ulichotenda. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Haukuongeza uchafu juu ya machukizo yako yote?


Lakini ninyi munasema: Matendo ya Yawe si sawa! Musikilize sasa, enyi Waisraeli: Ninachofanya mimi si sawa? Munachofanya ninyi ndicho kisichokuwa sawa.


Kisha Mungu akaniambia: Wewe mwanadamu, umeona mambo wazee wa Waisraeli wanayotenda kwa uficho, kila mutu katika chumba chake cha sanamu. Wanasema: Yawe hatuoni. Yawe ameiacha inchi.


Naye akaniambia: Uovu wa Waisraeli na watu wa Yuda ni mukubwa sana. Inchi imejaa umwagaji wa damu na katika muji hakuna haki, kwa maana wanasema: Yawe ameiachilia inchi; Yawe haoni.


Sasa basi, nitawagandamizia chini, kama gari lililojaa ngano.


Wakati huo nitauchunguza Yerusalema kwa taa, nitawaazibu wanaoishi wakitulia kama machicha ya divai, wote ambao wanasema kati yao: Yawe hatafanya kitu: chema au kibaya.


Munauliza: Mbona sasa hazikubali? Yawe hazikubali kwa sababu anajua wazi kwamba umeivunja ahadi yako kwa muke wa ujana wako. Umekosa uaminifu kwake ingawa uliahidi mbele ya Mungu kwamba ungekuwa mwaminifu kwake.


Ninawajibia hivi: Ni sawa kwa mutu kumudanganya Mungu? Hapana! Lakini ninyi munanidanganya! Ingawa hivyo ninyi munauliza: Tunakudanganya kwa namna gani? Kweli! Munanidanganya juu ya zaka na sadaka zenu.


Yawe ni mulima wa usalama. Kazi zake ni kamilifu, njia zake zote ni za haki. Yeye ni Mungu mwaminifu asiyekuwa na kosa, yeye anafanya mambo ya usawa na ya haki.


Muache kujisifu, muache kusema kwa kiburi. Maana anayejua ni Yawe. Yeye anayapima matendo yote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ