Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Malaki 2:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Munauliza: Mbona sasa hazikubali? Yawe hazikubali kwa sababu anajua wazi kwamba umeivunja ahadi yako kwa muke wa ujana wako. Umekosa uaminifu kwake ingawa uliahidi mbele ya Mungu kwamba ungekuwa mwaminifu kwake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Malaki 2:14
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha Yawe Mungu akasema: “Si vizuri huyu mwanaume kuwa peke yake. Nitamufanyia musaidizi wa kumufaa.”


Kama ukitesa wabinti zangu, au ukioa wanawake wengine zaidi ya hawa, basi ujue kwamba hakuna anayekuwa mushuhuda kati yetu ila Mungu mwenyewe.”


mwanamuke anayemwacha mwenzake wa ujana wake, na kusahau agano la Mungu wake.


Mwenendo wa mwanamuke mwasherati ni hivi: yeye anakula, anajipanguza mudomo, na kusema: “Sijafanya kosa lolote!”


Mwana wangu, kwa nini kutekwa na mwanamuke mwasherati? Kwa nini kukumbatia mwanamuke mugeni katika kifua?


Furahia maisha pamoja na muke wako unayemupenda muda wote wa maisha yako ya bure ambayo Mungu amekujalia hapa chini ya jua, maana hilo ndilo ulilopangiwa katika maisha, katika kutoa jasho yako hapa chini ya jua.


Hakika sura yako ni nzuri, ee mupenzi wangu, hakika sura yako ni nzuri! Macho yako ni kama ya njiwa!


Yerusalema, Yawe amekuita tena. Ulikuwa kama vile muke aliyeachwa na kuhuzunika. Mungu wako anasema: Muke aliyeolewa akiwa kijana, anaweza kuachiliwa?


Ninyi munaniuliza: Kwa nini tunafunga kula lakini wewe hauoni? Mbona tunajitesa, lakini wewe haujali? Ukweli ni kwamba wakati munapofunga kula, munatafuta tu furaha yenu wenyewe na kuwagandamiza watumishi wenu!


Jambo hili litawafikia kwa sababu wametenda katika Israeli mambo yasiyofanyika. Walizini na wake za jirani zao, na kusema maneno ya uongo kwa jina langu, jambo ambalo mimi sikuwaamuru wafanye. Mimi ninajua hayo. Nimeyashuhudia. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kisha, watu wakamwambia Yeremia: Yawe akuwe mushuhuda wa kweli na mwaminifu juu yetu ikiwa hatutafanya jinsi Yawe, Mungu wako atakavyokuagiza utuambie.


Walisikia haya walipotenda machukizo hayo? Hapana, hawakusikia haya hata kidogo. Hata zamiri hazikuwagonga. Kwa hiyo, wataanguka pamoja na wale walioanguka; nitakapowaazibu, wataangamia. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Ndimi zao ni hatari kama pinde; wameimarika kwa ajili ya uongo na si kwa ajili ya haki. Wanaendelea kutenda uovu kisha uovu, wala hawanitambui mimi. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Nilipopita tena karibu nawe, nikakuona. Wakati huu, ulikuwa umefikia umri wa kupendwa kama binti. Nikalitandaza vazi langu juu yako na kuufunika uchi wako. Nikafanya nawe agano la ndoa, nawe ukakuwa wangu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Musikilize enyi watu wote; sikiliza ewe dunia na vyote vinavyokuwa ndani yako. Bwana wetu Yawe anakuja kuwashitaki, Bwana wetu anasema kutoka hekalu lake takatifu.


Mungu hakuwafanya ninyi wote wawili mukuwe mwili mumoja na roho moja? Alikusudia nini alipofanya hayo? Tuzae watoto wanaomupendeza Mungu. Kwa hiyo, muchunge uzima wenu na kuhakikisha kwamba hakuna hata mumoja wenu anayekosa uaminifu kwa muke wake.


Yawe wa majeshi anasema: Kisha nitawakaribia kwa kuwahukumu. Sitasita kutoa ushuhuda juu ya wachawi, wazinzi, watoa ushuhuda wa uongo, wanaopunja mushahara wa watumishi, wanaowatesa wajane na wayatima, wanaozuia mugeni asipate haki yake na wale wasioniogopa mimi.


Ninawajibia hivi: Ni sawa kwa mutu kumudanganya Mungu? Hapana! Lakini ninyi munanidanganya! Ingawa hivyo ninyi munauliza: Tunakudanganya kwa namna gani? Kweli! Munanidanganya juu ya zaka na sadaka zenu.


Wale wazee wa Gileadi wakamwambia Yefuta: “Yawe atakuwa mushuhuda kati yetu. Hakika tutafanya kama ulivyosema.”


Samweli akajibu: “Yawe ni mushuhuda juu yenu, na mufalme wake muchaguliwa leo ni mushuhuda kuwa mumeniona sina kosa.” Wao wakajibu: “Yeye ni mushuhuda.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ