Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Malaki 2:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Yawe awatenge mbali watu wanaofanya mambo hayo kutoka kati ya wazao wa Yakobo. Na wasishiriki hata kidogo katika kutoa ushuhuda na kuleta sadaka mbele ya Yawe wa majeshi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Malaki 2:12
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakapiga kura juu ya utaratibu wa kazi, kwa wakubwa kama vile kwa wadogo, kwa walimu kama vile kwa wanafunzi. Haya ndiyo majina ya wakubwa wa vikundi ambao kura iliwaangukia: ya kwanza: Yosefu wa jamaa ya Asafu; ya pili: Gedalia ya tatu: Zakuri ya ine: Isiri ya tano: Netania ya sita: Bukia ya saba: Asarela ya nane: Yesaya ya kenda: Matania ya kumi: Simei ya kumi na moja: Azareli ya kumi na mbili: Hasabia ya kumi na tatu: Sebueli ya kumi na ine: Matitia ya kumi na tano: Yeremoti ya kumi na sita: Hanania ya kumi na saba: Yosibekasa ya kumi na nane: Hanani ya kumi na kenda: Maloti ya makumi mbili: Eliyata ya makumi mbili na moja: Hotiri ya makumi mbili na mbili: Gidalti ya makumi mbili na tatu: Mahasioti ya makumi mbili na ine: Romamuti-Ezeri Kila mukubwa pamoja na watu wengine wa jamaa yake walikuwa kikundi kimoja cha watu kumi na wawili.


Mimi Yawe ninapenda watu wafuate sheria yangu; ninachukia unyanganyi na uovu. Nitawatunza watu wangu kwa uaminifu, nitafanya nao agano la milele.


Lakini watu hawa wanafanya wanavyotaka: wananitolea sadaka ya ngombe na tena wanaua watu kwa kutambikia. Wananitolea sadaka ya mwana-kondoo na vilevile wanaua imbwa. Wananitolea sadaka ya unga na vilevile wanatolea damu ya nguruwe. Wanachoma ubani mbele yangu na kwenda kuabudu miungu ya uongo. Hao wamechagua kufuata njia zao wenyewe.


Nitamwazibu yule nabii pamoja na yule mutu aliyekuja kumwuliza mapenzi yangu; wote watapata azabu ileile.


Uwaambie Waisraeli kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitalichafua hekalu langu, hiyo nyumba ambayo munajivunia na kuitegemea na ambao munafurahi sana kuiona.


Hata kama wakilea watoto, sitamwacha hata mumoja wao muzima. Ole kwao, nitakapowaacha peke yao!


Watu wote watakaofanya mambo hayo ya kuchukiza wanapaswa kutengwa mbali na watu wao.


Mimi mwenyewe nitamukasirikia mutu huyu na kumutenga na watu wake kwa sababu alimutoa mumoja wa watoto wake sadaka kwa mungu Moleki na hivyo akachafua Pahali pangu Patakatifu na jina langu takatifu.


Hata mukinitolea sadaka zenu za kuteketezwa kwa moto na za vyakula, mimi sitakubali kuzipokea; na sadaka zenu za amani za nyama wanono mimi sitaziangalia kabisa.


Nami Yawe nitasaidia kwanza jamaa za Yuda kusudi wazao wa Daudi na wakaaji wa Yerusalema wasijione kuwa wenye utukufu zaidi kuliko watu wengine wa kabila la Yuda.


Heri kungepatikana mutu mumoja kati yenu ambaye angefunga milango ya hekalu kusudi musiwashe moto usiokubaliwa kwenye mazabahu yangu! Sipendezwi nanyi na sitaikubali sadaka yoyote munayonitolea.


Munasema: Mambo haya yametuchokesha sana na munanizarau. Munaniletea sadaka za nyama muliopata kwa njia ya kunyanganya, au wanaokua vilema au wagonjwa. Basi, nipokee sadaka hizo toka katika mikono yenu?


Sisi wote si watoto wa baba mumoja? Sisi wote hatukuumbwa na Mungu yuleyule? Mbona basi, hatuaminiani sisi kwa sisi, na tunalizarau agano Yawe alilofanya na babu zetu?


Hema zenu zinapendeza sana, enyi watu wa Yakobo; hakika, kambi zenu, enyi watu wa Israeli!


Muwaache! Wao ni vipofu, wanaongoza vipofu wengine. Na kama kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, wote wawili wanatumbukia ndani ya shimo.”


Lakini watu waovu na wadanganyifu wataendelea katika maovu, wakipotosha watu wengine na kujipotosha wenyewe.


Yule nyama akakamatwa pamoja na yule nabii wa uongo aliyeonyesha vitambulisho mbele yake. (Ni kwa njia ya vitambulisho vile aliwadanganya wale waliopigwa chapa ya yule nyama na wale walioabudu sanamu yake.) Nyama yule pamoja na nabii wa uongo wakatupwa wangali wazima katika ziwa la moto munamowaka mawe ya kiberiti.


Kwa hiyo ninaapa juu ya jamaa ya Eli kwamba uovu wao hautaondolewa hata kidogo kwa matoleo wala kwa sadaka.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ