Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Malaki 2:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Sisi wote si watoto wa baba mumoja? Sisi wote hatukuumbwa na Mungu yuleyule? Mbona basi, hatuaminiani sisi kwa sisi, na tunalizarau agano Yawe alilofanya na babu zetu?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Malaki 2:10
50 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ee Mungu, kumbuka jinsi watu walivyochafua ukuhani na agano la kikuhani na la Walawi.


Maana Mungu ndiye aliyeniumba mimi na mutumishi wangu; yeye ndiye aliyetuumba sisi wote.


Mujue kwamba Yawe ndiye Mungu. Yeye ndiye aliyetuumba, sisi ni mali yake; sisi ni watu wake na kondoo wake anaowachunga.


‘Ninyi wenyewe mumeona jinsi nilivyowatendea Wamisri na jinsi nilivyowapeleka ninyi kama vile tai anavyopeleka watoto wake kwa mabawa, nikawaleta kwangu.


Sasa basi, kama mukitii sauti yangu na kushika agano langu, mutakuwa watu wangu wachaguliwa kati ya mataifa yote, maana dunia yote ni yangu.


Basi, Musa akaenda na kuwaambia watu wote maneno na maagizo yote Yawe aliyomwambia. Watu wote wakajibu kwa sauti moja: Mambo yote Yawe aliyosema, tutayafanya.


Kisha akatwaa kitabu cha agano la Yawe, akakisoma mbele ya watu, nao wakasema: Yale yote Yawe aliyoyasema tutayafanya, nasi tutakuwa watiifu.


Yawe aliyewaumba enyi watu wa Yakobo, yeye aliyewafanya enyi watu wa Israeli, anasema hivi: Musiogope, maana mimi nimewakomboa; nimewaita kwa jina lenu nanyi ni wangu.


Mimi ni Yawe, Mutakatifu wenu; Mimi ndiye Muumba wa Israeli, Mufalme wenu.


Kila mumoja anajulikana kwa jina langu; niliwaumba wote na kuwafanya kwa ajili ya utukufu wangu.”


Mimi, Yawe Muumba wako, niliyekutengeza tangia tumbo la mama yako, ninakuja kukusaidia wewe. Mimi Yawe ninasema hivi: Musiogope, enyi wazao wa Yakobo, mutumishi wangu, usiogope, ewe Yeshuruni, muchaguliwa wangu.


Mukumbuke Abrahamu babu yenu, na Sara aliyewazaa ninyi. Abrahamu alikuwa hana mutoto wakati nilipomwita, lakini nilimubariki na kumufanya kuwa na wengi.


Maana wewe ndiwe Baba yetu; Abrahamu, babu yetu, hatujali, naye Israeli hatutambui; lakini wewe, ee Yawe, ni Baba yetu. Wewe umeitwa tangu zamani: Mukombozi wetu.


Hata hivyo, ee Yawe, wewe ni Baba yetu. Sisi ni kama udongo, wewe ni mufinyanzi. Sisi wote ni kazi ya mikono yako.


Usitukasirikie sana, ee Yawe, usiukumbuke uovu wetu siku zote! Ukumbuke kwamba sisi wote ni watu wako!


Watarudi wakiwa wanatoa machozi, nami nitawaongoza nikiwafariji; nitawapitisha kando ya vijito vya maji, katika njia iliyonyooka ambamo hawatajikwaa; maana mimi nimekuwa baba wa Israeli, Efuraimu ni muzaliwa wangu wa kwanza.


Wewe mwanadamu! Wakaaji waliobaki katika miji iliyoharibiwa katika inchi ya Israeli wanasema: Abrahamu alikuwa peke yake, hata hivyo, alipata kurizi inchi hii. Lakini sisi ni wengi; ni wazi tumepewa inchi hii ikuwe yetu!


Yawe wa majeshi anasema hivi: Mutoto anamuheshimu muzazi wake, na mutumishi anamuheshimu bwana wake. Ikiwa mimi ndiye Baba wenu, mbona munanivunjia heshima? Ikiwa mimi ni bwana wenu, mbona hamuniheshimu? Ninasema hivyo kwa ninyi makuhani munaozarau jina langu. Nanyi munauliza: Sisi tumezarau jina lako namna gani?


Watu wa Yuda wamekosa uaminifu kwa Mungu na kutenda machukizo katika Israeli na katika Yerusalema. Wamechafua hekalu la Yawe analolipenda. Tena wameoa wanawake wanaoabudu miungu ya kigeni.


Lakini ninyi makuhani mumegeuka na kuacha njia ya haki. Mafundisho yenu yamewaongoza watu wengi katika kutenda mabaya. Mumelivunja agano nililofanya nanyi.


“Ndugu atamutoa ndugu, kusudi auawe, na baba atamutoa mutoto wake, nao watoto watawageukia wazazi wao na kuwaua.


Halafu wakatuma kwake wamoja kati ya wanafunzi wao pamoja na watu wengine wamoja waliojiunga na Herode kumwuliza maneno haya: “Mwalimu, tunajua kuwa wewe ni mutu wa kweli na kwamba unafundisha kwa kweli njia Mungu anayoamuru. Vilevile haushuguliki na mafikiri ya mutu yeyote kwa sababu hauangalii cheo cha mutu.


Musijifikiri kwamba munaweza kujidai tu kuwa Abrahamu ndiye babu yenu. Ninawaambia kwamba Mungu anaweza kugeuza mawe haya kuwa watoto wa Abrahamu!


Basi muonyeshe kwa njia ya matendo kwamba mumegeuka toka zambi zenu. Musianze tu kujisemesha kwamba Abrahamu ndiye babu yenu. Ninawaambia kwamba Mungu anaweza kugeuza mawe haya kuwa watoto wa Abrahamu!


Wakamujibu: “Baba yetu ni Abrahamu.” Yesu akawaambia: “Kama mungekuwa watoto wa Abrahamu, basi mungefanya matendo yale Abrahamu aliyofanya.


Ninyi munafanya matendo yale baba yenu anayofanya.” Wakamujibu: “Sisi si watoto wa haramu. Tuko na baba mumoja, naye ndiye Mungu.”


Wewe ni mukubwa kuliko babu yetu Abrahamu? Yeye alikufa, na manabii walikufa vilevile. Wewe unajiona kuwa nani?”


Baba yenu Abrahamu alishangilia akitumainia kuona siku ya kuja kwangu; na wakati alipoiona, alifurahi.”


Mungu aliyeumba ulimwengu na vitu vyote vinavyokuwa ndani yake, yeye anayekuwa Bwana wa mbingu na dunia, hakai ndani ya hekalu zilizojengwa na watu.


Yeye hahitaji kushugulikiwa na watu, kama vile angekuwa na lazima ya musaada fulani. Kwa maana yeye ndiye anayewapa watu wote pumzi ya uzima, pamoja na vitu vyote wanavyohitaji.


Kutokana na mutu mumoja, yeye aliumba watu wa mataifa yote kusudi waishi katika dunia yote. Aliwapangia nyakati na kukata mipaka ya inchi wanayopaswa kukaa ndani yake.


Stefano akamujibu: “Wandugu zangu na wababa zangu, munisikilize! Mungu mwenye utukufu alimutokea babu yetu mukubwa Abrahamu wakati alipokuwa angali katika inchi ya Mesopotamia, mbele hajahamia katika muji Harani.


Kesho yake akawakutana Waisraeli wawili wakipigana, naye akajaribu kuwaamua, akiwaambia: ‘Warafiki, ninyi ni wandugu; kwa sababu gani munatendeana vibaya?’


Basi tuseme nini juu ya babu yetu Abrahamu? Nini iliyomutokea?


Na si vile tu; Rebeka alikuwa na watoto wawili aliowazaa na mume mumoja, ndiye babu yetu Isaka.


Ingawa hivi, kwa ngambo yetu sisi tuko na Mungu mumoja peke yake tu, ndiye Baba aliyeumba vitu vyote, nasi tunaishi kwa nguvu yake. Vilevile kuko Bwana mumoja tu, ndiye Yesu Kristo. Kwa njia yake vitu vyote viliumbwa, nasi tunaishi kwa nguvu yake.


Kwa hivi, muache uongo! Kila mumoja aseme ukweli kwa mwenzake, kwa maana sisi wote ni viungo vya mwili mumoja.


Mungu mumoja, Baba ya watu wote, anayekuwa juu ya wote, anayetumika kwa njia ya wote, na anayekaa ndani ya wote.


Kuelekea maneno hayo, mutu yeyote asimukosee ndugu yake wala kumudanganya. Tumekwisha kuwaambia na kuwahakikishia mbele kwamba Bwana atawaazibu wale wanaofanya mambo kama hayo.


Na ikiwa wababa zetu wa kimwili walituadibisha, nasi tuliwaheshimu, jambo hilo halionyeshi zaidi kwamba tunapaswa kumuheshimu Baba yetu wa kiroho na kupata kuishi?


Mimi Mungu nilimwondoa babu yenu Abrahamu kutoka kule ngambo ya muto Furati na kumuleta hapa Kanana, ambako nilimupatia wazao wengi. Nilimupa Isaka,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ